1Yawe anasema:
Piga kelele, wala usijizuize;
ulalamike kwa sauti kubwa kama baragumu.
Uwatangazie watu wangu makosa yao,
uwaambie wazao wa Yakobo zambi zao.
2Kila siku wananitafuta,
wanatamani kujua njia zangu,
kama vile wao ni taifa linalotenda haki,
taifa lisilosahau agizo la Mungu wao.
Wanataka niamue kwa haki,
na kutamani kuikaa karibu na Mungu.
3Ninyi munaniuliza:
Kwa nini tunafunga kula lakini wewe hauoni?
Mbona tunajitesa, lakini wewe haujali?
Ukweli ni kwamba wakati munapofunga kula,
munatafuta tu furaha yenu wenyewe
na kuwagandamiza watumishi wenu!
4Munafunga kula lakini munagombana na kupigana mangumi vikali.
Mukifunga namna hiyo,
maombi yenu hayatafika kwangu juu.
5Munapofunga kula, ninyi munajitaabisha;
munaviinamisha vichwa vyenu kama utete,
na kulalia nguo za magunia na majivu.
Hii ndio munayoita mafungo ya kula chakula?
Hiyo ni siku inayonipendeza mimi?
6Mafungo ninayotaka mimi ni haya:
kuwafungua waliofungwa bila haki,
kuziondoa kamba za utumwa,
kuwaacha huru wanaogandamizwa,
na kuvunja kabisa mambo yote ya kitumwa!
7Mafungo ya kweli ni kugawanya chakula chako pamoja na wenye njaa,
kuwakaribisha katika nyumba yako wamasikini wasiokuwa na makao,
kuwavalisha wasiokuwa na nguo,
bila kusahau kuwasaidia wandugu zenu.
8Mukifanya hivyo mutaonekana kama mwangaza wa mapambazuko,
na mutapona haraka.
Matendo yenu mema yatawatangulia,
nami nitawalinda kutoka nyuma kwa utukufu wangu.
9Halafu mutaomba,
nami Yawe nitawaitikia;
mutalia kwa sauti kwa kuomba musaada,
nami nitajibu hivi: Niko hapa!
Kama mukiondoa mambo ya kitumwa,
mukiacha kuzarau wengine na kusema maovu,
10mukiwapa wenye njaa chakula,
mukitimiza mahitaji ya wenye kuteswa,
mwangaza utawaangazia nyakati za giza,
giza lenu litakuwa kama muchana.
11Mimi Yawe nitawaongoza siku zote,
nitatimiza mahitaji yenu wakati wa shida.
Nitawaimarisha katika mwili,
nanyi mutakuwa kama bustani iliyomwangiliwa maji,
kama chemichemi ya maji
ambayo maji yake hayakauki hata kidogo.
12Watu wako watajenga tena mabomoko ya zamani;
mutajenga upya juu ya misingi iliyoachwa zamani.
Nanyi mutaitwa watu waliotengeneza upya kuta,
watu waliotengeneza tena barabara za miji.
Zawadi kwa ajili ya kuheshimu siku ya Sabato13Kama ukiacha kufanya kazi siku ya Sabato,
ukiacha shuguli zako siku yangu hiyo takatifu,
ukiifanya siku yangu kuwa ya furaha,
ukiheshimu siku hiyo takatifu ya Yawe,
ukiacha shuguli zako au kupiga domo,
14utapata furaha yako kwangu mimi Yawe,
nitakupatia ushindi katika kila upinzani katika inchi,
nitakulisha mali ya Yakobo, babu yako.
Maneno haya yanatoka katika kinywa cha Yawe.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.