1Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli waliokuwa viongozi wa jamaa, na majemadari wa maelfu na mamia na wakubwa wao waliomutumikia mufalme Daudi juu ya zamu za kuingia na kutoka. Kila mwezi katika mwaka, kundi tofauti la watu elfu makumi mbili na ine walishika zamu ya kufanya kazi.
2-15Walikuwa chini ya usimamizi wa wakubwa hawa:
Mwezi wa kwanza: Yasobeamu mwana wa Zabudieli, wa uzao wa Peresi. Alikuwa mukubwa wa majemadari wote wa jeshi katika mwezi wa kwanza.
Mwezi wa pili: Dodayi wa Ahoa. Alisaidiwa na jemadari Mikiloti.
Mwezi wa tatu: Benaya, mwana wa Yehoyada aliyekuwa Kuhani Mukubwa. Huyu ndiye Benaya aliyekuwa mutu shujaa katika kundi la watu makumi tatu na kiongozi wa kundi lile. Naye Amizabadi mwana wake, alikuwa jemadari.
Mwezi wa ine: Asaheli, ndugu ya Yoabu, na nyuma yake alifuatwa na Zebadia mwana wake.
Mwezi wa tano: Samuhuti wa uzao wa Isira.
Mwezi wa sita: Ira mwana wa Ikesi wa muji wa Tekoa.
Mwezi wa saba: Helesi wa muji wa Peloni, wa uzao wa Efuraimu.
Mwezi wa nane: Sibekayi wa muji wa Husati, wa uzao wa Zera.
Mwezi wa kenda: Abiezeri wa muji wa Anatoti wa uzao wa Benjamina.
Mwezi wa kumi: Maharai wa muji wa Netofati wa uzao wa Zera.
Mwezi wa kumi na moja: Benaya wa muji wa Piratoni.
Mwezi wa kumi na mbili: Heldai wa muji wa Netofati, wa uzao wa Otinieli.
Utawala wa makabila za Israeli16-22Haya ndiyo majina ya wakubwa wa kabila za Waisraeli:
Kabila la Rubeni: Eliezeri mwana wa Sikiri.
Kabila la Simeoni: Sefatia mwana wa Maka.
Kabila la Lawi: Hasabia mwana wa Kemueli.
Kabila la Haruni: Zadoki.
Kabila la Yuda: Elihu, mumoja wa wandugu za mufalme Daudi.
Kabila la Isakari: Omuri mwana wa Mikaeli.
Kabila la Zebuluni: Isimaya mwana wa Obadia.
Kabila la Nafutali: Yeremoti mwana wa Azrieli.
Kabila la Efuraimu: Hosea mwana wa Azazia.
Nusu ya kabila la Manase: Yoeli mwana wa Pedaya.
Nusu ya kabila la Manase katika Gileadi: Ido mwana wa Zekaria.
Kabila la Benjamina: Yasieli mwana wa Abeneri.
Kabila la Dani: Azareli mwana wa Yerohamu.
23Mufalme Daudi hakuwahesabu wale waliokuwa chini ya umri wa miaka makumi mbili kwa maana Yawe aliahidi kuwaongeza Waisraeli kuwa wengi kama nyota za mbinguni. Wasimamizi wa mali za kifalme
25-31Hawa ni wasimamizi wa mali ya mufalme Daudi:
Azimaweti mwana wa Adieli alisimamia hazina za mufalme Daudi.
Yonatani mwana wa Usia alisimamia hazina zilizokuwa katika inchi, miji, vijiji na katika minara.
Ezeri mwana wa Kalebu alisimamia walimaji.
Simei wa muji wa Ramati alisimamia kazi ya mashamba ya mizabibu.
Zabudi wa muji wa Sifi alisimamia mazao ya mashamba ya mizabibu.
Bali-Hanani wa muji wa Gederi alisimamia mizabibu na mikuyu ya inchi ya Shefela.
Yoasi alisimamia gala za mafuta.
Sitirayi wa muji wa Saroni alisimamia makundi ya ngombe waliokuwa kule Sarani.
Safati wa muji wa Adilai alisimamia makundi ya ngombe waliokuwa katika mabonde.
Obili Mwisimaeli alisimamia ngamia.
Yedeya, Mumeronoti alisimamia punda dike.
Yasisi, Muhagri, alisimamia makundi ya kondoo.
Washauri wa mufalme Daudi32Yonatani, mujomba wa mufalme Daudi, alikuwa mushauri na mutu mwenye ufahamu na mwandishi.
Yehieli mwana wa Hakemoni aliwafundisha wana wa mufalme.
33-34Ahitofeli alikuwa mushauri wa mufalme. Ahitofeli alipokufa, alikombolewa na Yehoyada mwana wa Benaya na Abiatari.
Husai Mwarki, alikuwa rafiki ya mufalme.
Yoabu alikuwa jemadari wa jeshi la mufalme.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.