1Nyuma ya siku sita, Yesu aliwatwaa Petro, Yakobo na ndugu yake Yoane, na kuwapeleka kwenye mulima murefu. Nao walikuwa kule peke yao.
2Na kule sura ya Yesu ikageuka wazi mbele yao. Uso wake ukangaa kama jua, nazo nguo zake zikametameta kama mwangaza.
3Halafu Musa na Elia wakiwa wakisemezana na Yesu, wakawatokea wale wanafunzi.
4Basi Petro akamwambia Yesu: “Bwana, ni vizuri kuona kwamba sisi tuko hapa. Ukitaka, nitajenga hapa vibanda vitatu, kimoja chako, kimoja cha Musa na kingine cha Elia.”
5Naye alipokuwa angali akisema, wingu lenye kuangaza likawafunika, na sauti ikasikilika toka katikati ya lile wingu ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa, ninapendezwa naye sana. Mumusikilize!”
6Wanafunzi wale waliposikia sauti ile, wakaogopa sana, wakaanguka uso mpaka chini.
7Lakini Yesu akawajongelea, akawagusa na kuwaambia: “Musimame, musiogope.”
8Nao walipoinua macho yao, hawakumwona mutu mwingine, isipokuwa Yesu peke yake.
9Walipokuwa wakishuka toka kwa mulima, Yesu akawaamuru: “Musimwelezee mutu mambo muliyoona mpaka Mwana wa Mutu atakapofufuka.”
10Kisha wanafunzi wakamwuliza: “Kwa nini basi walimu wa Sheria wanasema kwamba sherti Elia arudi kwanza?”
11Yesu akawajibu: “Hakika Elia anapaswa kurudi kwanza kutengeneza mambo yote.
12Lakini ninawaambia kama Elia amekwisha kurudi, nao hawakumutambua, lakini walimutendea yote waliyotaka. Ni vile ndivyo Mwana wa Mutu atateswa nao vilevile.”
13Halafu wanafunzi wakafahamu kwamba alisema nao juu ya Yoane Mubatizaji.
Yesu anaponyesha mwenye kifafa(Mk 9.14-29; Lk 9.37-43a)14Yesu na wanafunzi wake waliendelea hata wakafika kwenye kundi la watu. Pale mutu mumoja akamwendea Yesu, akapiga magoti mbele yake,
15na kusema: “Bwana, ninakuomba umusikilie mwana wangu huruma kwa maana anateswa sana na ugonjwa wa kifafa. Mara nyingi anaanguka katika moto na ndani ya maji.
16Nilimuleta kwa wanafunzi wako, lakini hawakuweza kumuponyesha.”
17Na Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Ee ninyi watu wa kizazi kisichoamini Mungu na chenye kupotoka. Nitakaa pamoja nanyi tena mpaka wakati gani? Nitawavumilia tena mpaka wakati gani? Muniletee mutoto hapa.”
18Yesu akamukaripia yule pepo aliyekuwa ndani ya yule mutoto, naye akamwacha, na tangia saa ile ile yule mutoto akapona.
19Kisha wanafunzi wakamufikia Yesu, wakiwa peke yao, na kumwuliza: “Kwa nini sisi hatukuweza kumufukuza yule pepo?”
20Yesu akawajibu: “Kwa sababu imani yenu ni ndogo. Kweli ninawaambia kama mukiwa na imani, hata ikiwa tu kama punje ndogo sana ya mbegu ya haradali, mutaweza kuuambia mulima huu: ‘Toka hapa uende kule,’ nao utatoka pale. Hakuna kitu chochote kitakachokosa kuwezekana kwenu.”
Yesu anajulisha tena habari za kufa na kufufuka kwake(Mk 9.30-32; Lk 9.43b-45)22Wanafunzi walipokuwa pamoja katika jimbo la Galilaya, Yesu akawaambia: “Mwana wa Mutu atatolewa katika mikono ya watu,
23nao watamwua, lakini kwa siku ya tatu kisha kufa kwake, atafufuka.” Halafu wanafunzi wakahuzunika sana.
Kulipa kodi ya hekalu24Yesu na wanafunzi wake walipofika katika muji Kapernaumu, walipishaji wa kodi ya hekalu wakamwendea Petro na kumwuliza: “Si mwalimu wenu analipa kodi ya hekalu?”
25Petro akawajibu: “Ndiyo, analipa.”
Petro alipoingia ndani ya nyumba, mbele hajasema kitu Yesu akamwuliza: “Simoni, unafikiri nini? Wafalme wa dunia wanawalipisha watu gani kodi au malipo mengine mbalimbali? Ni watu wa jamaa zao wenyewe au watu wengine?”
26Petro akamujibu: “Watu wengine.”
Na Yesu akamwambia: “Basi ni kusema kwamba watu wa jamaa zao wako na ruhusa ya kutolipa.
27Lakini haifai kuwakwaza. Kwa hiyo kwenda kwenye ziwa, na utupe ndoana ndani ya maji. Na samaki wa kwanza utakayemunasa, ufungue kinywa chake, nawe utaona kikoroti cha feza. Ukikamate na kukitoa kwa kulipa kodi kwa ajili yetu sisi wawili.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.