Kumbukumbu la Sheria 17 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1“Musitoe sadaka kwa Yawe, Mungu wenu, ngombe au kondoo mwenye kilema; hiyo ni chukizo kwa Yawe, Mungu wenu.

2“Kama mukisikia katika mumoja wa miji yenu kuna mwanaume au mwanamuke anayetenda maovu mbele ya Yawe, Mungu wenu, na kuvunja agano lake

3naye amekwenda na kutumikia miungu mingine na kuiabudu, akiabudu jua, mwezi au vitu vingine vya mbinguni nisivyoagiza,

4mutafanya uchunguzi kamili, na kama ni kweli kwamba kitu hiki kiovu kimefanywa katika Israeli,

5basi, mumupeleke mutu huyo inje ya miji na kumupiga mawe mpaka akufe.

6Hata hivyo, atauawa ikiwa kuna ushuhuda wa watu wawili au watatu. Asiuawe ikiwa kuna ushuhuda wa mutu mumoja tu.

7Wale washuhuda ndio watakaoanza kumupiga mawe kwanza, halafu wengine wamupige mawe. Ndivyo mutakavyokomesha uovu kati yenu.

8Inawezekana kutatokea mashitaki mengine yanayokuwa magumu ndani ya miji yenu, kama vile maneno yanayoelekea uchafu, mambo ya haki za watu, na hasara ya mwili. Basi, mutaondoka na kwenda pahali Yawe, Mungu wenu alipopachagua,

9na huko mutawaendea makuhani wa Kilawi, na mwamuzi ambaye yuko katika kazi kwa wakati huo, nanyi mutatoa mashitaki kwao nao watawatangazia uamuzi wao.

10Kisha mutafanya kama vile watakavyowatangazia pale pahali Yawe atakapochagua. Mutakuwa waangalifu kufanya yote kama vile watakavyowaagiza.

11Itawapasa kufanya kufuatana na maongozi watakayowapatia na uamuzi watakaotoa kwenu. Musiache kutimiza hukumu watakayowatangazia kwa kupita kuume au kushoto.

12Naye mutu atakayetenda kwa kiburi bila kutii kuhani aliyewekwa hapo kwa kumutumikia Yawe, Mungu wenu, au mwamuzi, mutu huyo atauawa. Ndivyo mutakavyokomesha uovu kati yenu.

13Watu wote watasikia na kuogopa wasifanye tena kitu kwa kiburi.

Maagizo juu ya mufalme

14“Mutakapokwisha kuingia katika inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, anawapa, mukirizi na kukaa humo, nanyi mukisema kwamba mutaweka mufalme juu yenu, kama vile mataifa yote yanayowazunguka,

15munaweza kumuweka mufalme juu yenu mutu ambaye Yawe, Mungu wenu, atamuchagua. Mutamuweka mumoja wa wandugu zenu kuwa mufalme juu yenu. Musimufanye mugeni asiyekuwa ndugu yenu kuwa mufalme wenu.

16Hata hivyo, asikuwe na farasi wengi kwa ajili yake mwenyewe, wala asiwarudishe watu Misri kwa kujipatia farasi zaidi, kwa sababu Yawe amewaonya: ‘Hamutarudi tena kwa njia ile.’

17Wala asijipatie wake wengi; kama sivyo moyo wake utaasi. Wala asijipatie feza na zahabu kwa wingi sana.

18Atakapokuwa akiikalia kiti cha ufalme anapaswa kuandika mufano wa sheria hii katika kitabu kinachokuwa mbele ya makuhani wa Kilawi.

19Mufano huo atakuwa nao siku zote na kuusoma maisha yake yote, kusudi apate kujifunza kumwogopa Yawe, Mungu wake, akishika na kutimiza maneno yote ya sheria hii na masharti haya,

20bila kujitukuza mwenyewe juu ya wandugu zake, wala kuiweka kando amri hii kwa namna yoyote, kusudi aweze kudumu katika utawala, yeye na wazao wake katika Israeli.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help