Yobu 26 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Jibu la Yobu

1Kisha Yobu akajibu:

2Aa! Jinsi gani ulivyomusaidia asiyekuwa na uwezo!

Jinsi gani ulivyomwokoa asiyekuwa na nguvu!

3Jinsi gani ulivyomushauri asiyekuwa na hekima,

na kumushirikisha ujuzi wako!

4Lakini umesema hayo kwa ajili ya nani?

Nani aliyekusukuma kuongea hivyo?

Bildadi anasema

5Mizimu kule chini inatetemeka,

maji ya chini na wakaaji wake yanaogopa.

6Kuzimu kuko wazi kabisa mbele ya Mungu.

Shimo la kuangamia halina kifuniko chochote.

7Mungu anatandaza kaskazini juu ya pahali patupu,

na anatundika dunia pahali pasipo kuwa kitu.

8Anayafunga maji katika mawingu yakuwe mazito,

nayo mawingu hayapasuki kwa uzito wake.

9Anaufunika uso wa mwezi

na kutandaza juu yake wingu.

10Amechora muviringo juu ya uso wa bahari,

penye mpaka kati ya mwangaza na giza.

11Mungu akitoa sauti ya kukaripa,

nguzo za mbingu zinatetemeka na kushangaa.

12Kwa nguvu zake alituliza bahari;

kwa maarifa yake alimwangamiza Rahabu.

13Kwa pumzi yake alisafisha anga;

mukono wake ulitoboa nyoka mukubwa anayeruka.

14Ikiwa haya ni machache tu ya matendo yake,

ni minongono tu tunayosikia juu yake,

nani anayeweza kujua ukubwa wa nguvu yake?

Yobu anaendelea kusema
Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help