1Ninakuamuru mbele ya Mungu na mbele ya Kristo Yesu atakayewahukumu wazima na wafu na kufuatana na kurudi kwake kwa kutawala:
2utangaze Neno la Mungu kwa nguvu kwa wakati unaofaa na kwa wakati usiofaa. Ukaripe, usahihishe na kuonya ukifundisha kwa uvumilivu.
3Maana kutakuja wakati watu watakapokataa kusikiliza mafundisho ya kweli, lakini watafuata tamaa zao wenyewe wakijitafutia walimu wengi kwa kuwafundisha mambo yale wanayotamani kusikia.
4Watafunga masikio yao wasisikilize mambo ya kweli na kusikiliza hadisi za uongo.
5Lakini wewe, ujiangalie katika mambo yote, uvumilie mateso, ufanye kazi yako ya kuhubiri Habari Njema na kutimiza kabisa utumishi wako.
6Kwa maana, mimi sasa niko tayari kutolewa kama sadaka, na wakati wa kufa kwangu umekaribia.
7Nimeshindana vizuri, nimekimbia na kufika mwisho wa mashindano yangu. Nimelinda imani yangu.
8Tangia sasa nimetayarishiwa zawadi ya ushindi, ndiyo ile taji ya haki, ambayo Bwana anayekuwa Mwamuzi wa haki atakayonipa siku ile ya kurudi kwake. Wala hatanipa mimi peke yangu tu, lakini na wale wote wanaopenda kumwona wakati atakaporudi.
Maagizo mbalimbali ya pekee9Ufanye nguvu kufika kwangu upesi.
10Dema amependelea mambo ya dunia hii akaniacha na kwenda Tesalonika. Kreske akaenda Galatia, na Tito akaenda Dalmatia.
11Luka peke yake ndiye anayekuwa hapa pamoja nami. Umutwae Marko, ukuje pamoja naye, kwa sababu ananifalia katika kazi yangu.
12Nimemutuma Tikiko kule Efeso.
13Wakati utakapokuja uniletee koti niliyoacha kule Troa kwa Karpo; uniletee vilevile vitabu, hasa vile vya ngozi.
14Alesanduro, yule mufua vyuma amenitendea mabaya mengi. Bwana atamulipa kufuatana na matendo yake.
15Nawe vilevile ujilinde naye kwa sababu alipinga kwa nguvu maneno yetu yote.
16Nilipojitetea kwa mara ya kwanza hakuna hata mutu mumoja aliyenisaidia; wote waliniachilia. Mungu asiwahesabie makosa yao!
17Lakini Bwana alinisaidia, akanitia nguvu nipate kuitangaza Habari Njema kwa ukamilifu kusudi watu wa mataifa mengine wapate kuisikia. Nami nikaokolewa toka katika kinywa cha simba.
18Bwana ataniokoa toka katika mambo yote mabaya na kunipeleka salama katika Ufalme wake wa mbinguni. Bwana atukuzwe milele na milele. Amina.
Salamu19Unisalimie Prisila na Akila na jamaa la Onesiforo vilevile.
20Erasto alibakia Korinto, na nilimwacha Trofimo kule Mileto kwa sababu alikuwa mugonjwa.
21Ufanye nguvu kufika mbele ya wakati wa baridi kali.
Eubulo, Pude, Lino, Klaudia na wandugu wote waamini wanakusalimia.
22Bwana akulinde.
Ninawatakia neema kutoka kwa Mungu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.