1Barua hii inatoka kwangu mimi Yakobo, mutumishi wa Mungu na wa Bwana Yesu Kristo. Ninawasalimia ninyi watu wa makabila kumi na mawili waliosambazwa katika dunia.
Imani na hekima2Wandugu zangu, muhesabu kuwa ni jambo la furaha sana wakati munapopata majaribu ya namna mbalimbali,
3kwa maana munajua kwamba kupimwa kwa imani yenu kunawaletea uvumilivu.
4Lakini sherti uvumilivu ule utimize kazi yake, kusudi mupate kuwa wakamilifu na watimilifu wasiopungukiwa na kitu.
5Kama mumoja kati yenu akikosa kuwa na hekima, aiombe kwa Mungu ambaye atamupatia. Kwa maana Mungu anawapa watu wote bila upendeleo na kwa moyo mwema.
6Lakini inafaa aombe kwa imani pasipo kuwa na mashaka. Kwa maana mutu anayekuwa na mashaka anafanana na zoruba katika bahari inayosukumwa na upepo na kutupa maji huku na huko.
7Mutu wa namna hiyo asizani kwamba atapokea kitu chochote kutoka kwa Bwana,
8kwa sababu ni mutu wa nia mbili, na mwenye kugeukageuka katika mwenendo wake.
Umasikini na utajiri9Ndugu anayekuwa masikini afurahi kwa sababu Mungu anamupandisha,
10na ndugu anayekuwa tajiri afurahi kwa sababu Mungu anamushusha. Maana tajiri atatoweka kama maua ya pori.
11Jua linatokea na kwa joto kali linakausha mimea, nayo maua yake yanaanguka na uzuri wake wote unaharibika. Hivi ndivyo tajiri naye atakavyotoweka katika shuguli zake.
Vipimo na majaribu12Heri mutu yule anayevumilia wakati anapojaribiwa, kwa maana akiisha kushinda majaribu, atapokea ile taji ya uzima ambayo Mungu aliahidia wale wanaomupenda.
13Wakati mutu anapojaribiwa, asiseme hivi: “Ninajaribiwa na Mungu!” Kwa maana Mungu hawezi kujaribiwa na ubaya, wala yeye mwenyewe hawezi kumujaribu mutu.
14Lakini kila mutu anajaribiwa wakati anapovutwa na kudanganywa na tamaa yake mbaya mwenyewe.
15Halafu ile tamaa mbaya ikisha kukomaa, inazaa zambi, nayo zambi ikisha kukomaa inazaa lufu.
16Wandugu zangu wapendwa, musidanganyike!
17Kila zawadi nzuri na kila zawadi kamilifu inatoka juu kwa Mungu Baba aliyeumba miangaza yote inayokuwa katika mbingu. Mungu hawezi kubadilika wala kugeuka.
18Kwa mapenzi yake mwenyewe alitupatia sisi uzima kwa njia ya ujumbe wa kweli, kusudi tupate kuwa kama mavuno ya kwanza katikati ya viumbe vyake.
Kusikia na kutenda19Wandugu zangu wapendwa, mukumbuke neno hili: kila mutu anapaswa kuwa mwepesi kwa kusikia, lakini asikuwe mwepesi kwa kusema na kukasirika.
20Kwa maana mutu mwenye kasirani hawezi kutimiza mambo ya haki mbele ya Mungu.
21Kwa sababu hiyo, mutupilie mbali mambo yote machafu na matendo ya uovu yanayozidi. Mupokee kwa unyenyekevu neno lile lililopandwa ndani yenu na linaloweza kuwaokoa.
22Musijidanganye ninyi wenyewe kwa kusikiliza tu neno la Mungu, lakini mulitimize kwa matendo.
23Kwa maana mutu anayesikia neno tu pasipo kulitimiza, anafanana na mutu anayejiangalia sura yake mwenyewe katika kioo.
24Kisha kujiangalia, anajiendea, na mara moja anasahau namna anavyokuwa.
25Lakini mutu anayechunguza sheria kamilifu inayoweka watu huru na kuendelea kushikamana nayo, na si kuisikia tu na kisha kuisahau, lakini anaitimiza kabisa, mutu huyu atabarikiwa na Mungu katika shuguli zake.
26Kama mutu akizani kwamba yeye ni mutu wa dini naye hawezi kuzuiza ulimi wake, anajidanganya mwenyewe, nayo dini yake haina faida.
27Dini inayokuwa safi na bila kosa mbele ya Mungu Baba ndiyo hii: kushugulikia wayatima na wajane wanaoteswa, na kujilinda mwenyewe na uchafu wa dunia hii.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.