1Kisha Yobu akamujibu Yawe:
2Ninajua kwamba unaweza kila kitu,
lolote unalokusudia haliwezi kuzuiliwa.
3Ulisema kwamba nilivuruga mipango yako bila akili.
Kweli nilitamka kitu ambacho sikuelewa,
mambo ya ajabu sana kwangu
ambayo sikukuwa ninayajua.
4Uliniambia nisikilize nawe utaniambia;
kwamba utaniuliza nami nikujibu.
5Kweli nilikuwa nimesikia habari zako kwa masikio tu,
lakini sasa ninakuona kwa macho yangu mwenyewe.
6Kwa hiyo ninatubu na kujihukumu;
ninajinyenyekeza na kuikaa juu ya mavumbi na majivu.
Mwisho wa habari ya Yobu7Yawe alipomaliza kuongea na Yobu, akamwambia Elifasi wa inchi ya Temani: “Kasirani yangu imewaka juu yako na warafiki zako wawili maana hamukusema ukweli juu yangu kama vile mutumishi wangu Yobu alivyofanya.
8Kwa hiyo mutwae ngombe dume saba na kondoo dume saba, muende kwa mutumishi wangu Yobu, mutoe nyama wale kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa ajili yenu. Naye mutumishi wangu Yobu atawaombea, nami nitaisikiliza maombi yake na kuacha kuwatendea kulingana na upumbafu wenu; maana hamukusema ukweli juu yangu kama mutumishi wangu Yobu alivyofanya.”
9Basi, Elifasi wa inchi ya Temani, Bildadi wa inchi ya Shua, na Zofari wa inchi ya Namati, wakafanya kama vile Yawe alivyowaambia. Yawe akapokea maombi ya Yobu.
10Nyuma ya Yobu kuwaombea warafiki zake, Yawe akamurudishia Yobu hali yake ya kwanza. Akamupa mara mbili ya yote aliyokuwa nayo pale mbele. Ang. Yobu 1.1-3
11Kisha wandugu zake, wadada zake na warafiki wote waliomufahamu mbele wakamwendea kwake, wakakula chakula pamoja naye. Wakamupa pole na kumufariji kwa ajili ya mateso yote ambayo Yawe alikuwa amemuletea. Kila mumoja wao akamupa Yobu feza na pete ya zahabu.
12Katika miaka ya Yobu iliyofuata, Yawe alimubariki zaidi kuliko hata alivyokuwa amemubariki pale mbele. Basi Yobu akakuwa na kondoo elfu kumi na ine, ngamia elfu sita, ngombe elfu mbili na punda dike elfu moja.
13Alikuwa vilevile na watoto wanaume saba na wabinti watatu.
14Binti yake wa kwanza alimupa jina Yemima, wa pili Kezia, na wa mwisho Kereni-Hapuki.
15Katika inchi yote hiyo hakukukuwa wanawake waliokuwa wazuri kama vile wabinti wa Yobu. Baba yao akawaachia urizi kama vile alivyowaachia kaka zao.
16Nyuma ya pale, Yobu aliishi miaka mia moja makumi ine, akawaona vijukuu na vitukuu vyake vyote mpaka kizazi cha ine.
17Basi, Yobu akakufa akiwa muzee wa miaka mingi.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.