Zaburi 105 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Mungu na watu wake(1 Sik 16.8-22)

1Mumushukuru Yawe,

mutangaze ukubwa wake,

mujulishe mataifa mambo aliyotenda!

2Mushangilie,

mumwimbie Mungu sifa,

mueleze matendo yake ya ajabu!

3Mujisifu kwa ajili ya jina lake takatifu;

wanaomutafuta Yawe wafurahi.

4Mumutafute Yawe mwenye nguvu;

mumutafute Yawe siku zote.

5Mukumbuke matendo ya ajabu aliyotenda,

miujiza yake na hukumu alizotoa,

6enyi wazao wa Abrahamu mutumishi wake,

enyi wazao wa Yakobo muchaguliwa wake.

7Yeye ndiye Yawe, Mungu wetu;

hukumu zake zina nguvu katika dunia yote.

8Yeye anashika agano lake milele,

anatimiza ahadi zake kwa vizazi elfu.

9Anashika agano alilofanya na Abrahamu,

na ahadi aliyomwapia Isaka.

10Alimusimamishia Yakobo ahadi yake,

akamuhakikishia agano hilo la milele.

11Alisema: “Nitawapa inchi ya Kanana,

nayo itakuwa mali yenu wenyewe.”

12Watu wa Mungu walikuwa wachache tu,

tena walikuwa wageni katika inchi ya Kanana.

13Walitangatanga kutoka taifa mpaka taifa,

kutoka inchi moja mpaka inchi ingine.

14Lakini Mungu hakuruhusu wateswe;

kwa ajili yao aliwaonya wafalme, akisema:

15“Musiwaguse wachaguliwa wangu;

musiwazuru manabii wangu!”

16Mungu alileta njaa katika inchi yao,

akafunga njia zao zote za kupata chakula.

17Lakini aliwatangulizia mutu mumoja,

Yosefu aliyekuwa ameuzishwa kuwa mutumwa.

18Walimufunga miguu kwa minyororo,

na kikomo cha chuma kwenye shingo,

19mpaka kile alichotabiri kilipotimia.

Neno la Yawe likahakikisha kwamba alikuwa na haki.

20Mufalme wa Misri akaamuru afunguliwe;

mutawala wa mataifa akamwachilia huru.

21Alimuweka kuwa musimamizi wa serikali yake,

na mukubwa wa mali yake yote,

22awaongoze wakubwa wa serikali yake sawa anavyopenda,

na kuwafundisha wazee wake hekima.

23Halafu Israeli akaingia katika inchi ya Misri;

Yakobo akakuwa mugeni katika inchi ya Hamu.

24Yawe akawafanya watu wake wazae sana;

akawajalia nguvu kuliko waadui zao.

25Aliwafanya Wamisri wawachukie watu wake,

wakawatendea watumishi wake vibaya.

26Kisha akamutuma Musa mutumishi wake,

akamutuma pamoja na Haruni muchaguliwa wake.

27Wakafanya maajabu ya Mungu kati ya Wamisri,

na miujiza katika inchi hiyo ya Hamu.

28Mungu akaleta giza juu ya inchi;

lakini Wamisri wakakataa kutii amri zake.

29Akageuza mito yao kuwa damu,

akaua samaki wao wote.

30Vyura wakajaa juu ya inchi yao,

hata katika nyumba ya mufalme.

31Mungu akaamuru, kukatokea makundi ya mainzi,

na imbu katika inchi yote.

32Kwa pahali pa mvua akawatumia mvua ya mawe,

na radi iliyounguza inchi yao yote;

33akaharibu mizabibu na miti yao ya tini;

akavunja miti ya inchi yao.

34Mungu akaamuru, kukatokea nzige,

na mapanzi maelfu yasiyohesabiwa;

35wakatafuna mimea yote katika inchi,

wakakula mazao yao yote.

36Aliua wazaliwa wa kwanza katika inchi yao,

ndilo chipukizi la kwanza la jamaa za Wamisri.

37Kisha akawaondoa watu wa Israeli katika inchi,

wakikuwa na feza na zahabu;

wala hakuna hata mumoja wao aliyejikwaa.

38Wamisri walifurahia kuondoka kwao,

maana hofu iliwashika kwa sababu yao.

39Mungu alitandaza wingu juu ya watu wake,

na moto kusudi uwaangazie usiku.

40Waliomba, naye akawaletea kwale,

akawapa mukate kutoka mbinguni kwa wingi.

41Alipasua jiwe maji yakabubujika;

yakatiririka katika jangwa kama muto.

42Alikumbuka ahadi yake takatifu

aliyomupa Abrahamu mutumishi wake.

43Basi akawaondoa watu wake katika inchi,

wachaguliwa wake wakaimba na kushangilia.

44Aliwapa inchi za mataifa

na kuwatolea mashamba ya wenyeji,

45kusudi watu wake watii masharti yake,

na kufuata sheria zake.

Haleluia!

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help