1Wakati mufalme Daudi alipokuwa akiikaa katika nyumba yake ya kifalme, siku moja akamwita nabii Natani, na kumwambia: “Angalia, mimi ninakaa katika nyumba nzuri iliyojengwa na miti ya mwerezi, lakini Sanduku la Agano la Yawe linakaa ndani ya hema.”
2Natani akamwambia Daudi: “Ufanye chochote unachofikiri ndani ya moyo wako, maana Mungu yuko pamoja nawe.”
3Lakini usiku uleule, neno la Yawe lilimufikia Natani kusema hivi:
4“Kwenda umwambie mutumishi wangu Daudi: Yawe anasema hivi: Wewe hautanijengea nyumba ya kukaa.
5Tangu wakati ule nilipowaongoza watu wa Israeli kutoka Misri mpaka hivi leo, sijaishi katika nyumba. Nimekuwa nikihama toka hema hata hema, na toka makao hata makao mengine.
6Kila pahali nilipokwenda na Waisraeli, sikupata hata mara moja kuwauliza waamuzi wao niliowaamuru wachunge watu wangu, ‘Kwa nini haukunijengea nyumba ya mierezi?’
7“Kwa hiyo basi, umwambie mutumishi wangu Daudi: Yawe wa majeshi anasema hivi: Nilikutoa katika shamba la malisho ulipokuwa unachunga kondoo, kusudi ukuwe mukubwa wa watu wangu Waisraeli.
8Tangu wakati ule nimekuwa pamoja nawe kokote ulikokwenda na nimewaangamiza waadui zako wote mbele yako. Nitakufanya kuwa mwenye heshima kama vile wakubwa wengine wa dunia.
9Nami nitawachagulia watu wangu wa Israeli pahali pa kuishi niwapandikize, kusudi waishi pahali pao wenyewe, wasisumbuliwe tena. Nao watu wakali wanaotumia nguvu hawatawatesa tena kama zamani,
10wakati nilipowachagua waamuzi juu ya watu wangu Waisraeli. Mimi nitawashinda waadui zako wote. Zaidi ya yote, mimi Yawe ninakutangazia kwamba nitakupa wazao.
11Siku zako zitakapotimia za kujiunga na babu zako, nitamufanya mumoja wa watoto wako wewe mwenyewe akuwe mufalme; nami nitaimarisha ufalme wake.
12Yeye ndiye atakayenijengea nyumba; nami nitahakikisha kwamba ufalme wake unadumu milele.
13Mimi nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwana wangu. Sitaacha kumutendea mema kama vile nilivyoacha kumutendea Saulo aliyekutangulia. Ang. 2 Kor 6.18; Ebr 1.5
14Lakini nitamwimarisha katika nyumba yangu na katika ufalme wangu milele, na kiti chake cha kifalme kitakuwa imara siku zote.”
15Natani akamwelezea Daudi mambo hayo yote kulingana na maono hayo.
Maombi ya Daudi ya shukrani(2 Sam 7.18-29)16Kisha mufalme Daudi akaingia ndani ya hema na kuikaa mbele ya Yawe, halafu akaomba: “Mimi ni nani, ee Yawe Mungu, na nyumba yangu ni nini hata unitukuze hivi?
17Tena jambo hili lilikuwa dogo mbele ya macho yako, ee Mungu. Zaidi ya hayo, umenitolea ahadi juu ya vizazi vyangu vinavyokuja, ee Yawe Mungu!
18Nikuambie nini zaidi, mimi Daudi mutumishi wako, kwa kunitukuza vile? Wewe unanijua mimi mutumishi wako.
19Ee Yawe, kwa ajili ya mutumishi wako na kwa kufuatana na moyo wako mwenyewe, umeyatenda hayo makubwa yote, kusudi hayo matendo makubwa yote yajulikane.
20Hakuna mwingine kama wewe, ee Yawe, na yote tunayosikia yanahakikisha kwamba hakuna Mungu mwingine lakini wewe tu.
21Tena ni watu gani katika dunia ambao wanaweza kulinganishwa na watu wako Waisraeli? Hao ndio watu peke yao Mungu wao alikwenda kuwakomboa kusudi wakuwe watu wake. Ukajipatia sifa kwa kutenda mambo makubwa na ya ajabu pale ulipofukuza mataifa mbele ya watu wako ambao uliwakomboa kutoka Misri.
22Hata ukajifanyia watu wako Waisraeli kuwa watu wako milele; nawe ee Yawe, umekuwa Mungu wao.
23“Basi sasa, ewe Yawe, uimarishe milele neno lako ulilosema juu yangu mimi mutumishi wako na juu ya jamaa yangu.
24Nalo jina lako litatukuzwa milele, nao watu watasema: ‘Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, ndiye Mungu juu ya Israeli!’ Na jamaa yangu, mimi Daudi mutumishi wako, itaimarishwa mbele yako.
25Maana, ee Mungu wangu, nimepata bidii ya kukuomba kwa sababu umenifunulia ukisema kwamba utanipa wazao.
26Sasa ee Yawe, wewe ndiwe Mungu, umeniahidi mimi mutumishi wako jambo hili jema.
27Kwa hiyo ninakuomba ubariki wazao wangu, mimi mutumishi wako, kusudi wadumu milele mbele yako; maana unapobariki, baraka zako zinadumu milele.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.