Maombolezo 1 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Namna gani muji uliokuwa umejaa watu,

sasa unakaa peke yake!

Ulikuwa na utukufu kati ya mataifa,

sasa umekuwa kama mama mujane.

Ulikuwa kama binti wa mufalme kati ya miji,

sasa umekuwa mutumwa.

2Unalia usiku kucha;

machozi yanatiririka juu ya mashavu yake.

Hakuna hata mumoja kati ya wapenzi wake kwa kuufariji.

Rafiki zake wote wameudanganya;

wamekuwa waadui zake.

3Watu wa Yuda wamekwenda katika uhamisho,

wakijaa mateso na kuwa katika utumwa mukali.

Wanakaa kati ya watu wa mataifa,

wala hawapati nafasi ya kupumzikia.

Waliowafuatilia wamewakamata wakiwa katika taabu.

4Barabara za Sayuni zinaomboleza,

maana hakuna anayepita kwa sikukuu.

Milango yake yote ni tupu,

makuhani wake wanaugua,

wabinti zake wana huzuni,

na muji wenyewe uko katika uchungu.

5Waadui zake ndio wanaoutawala na wanafanikiwa,

maana Yawe ameutesa

kwa sababu ya makosa yake mengi.

Watoto wake wanapelekwa katika uhamisho.

6Utukufu wote wa watu wa Sayuni umetoweka;

wakubwa wake wamekuwa kama kulungu wasiokuwa na malisho.

Waliwakimbia watesi wao bila nguvu.

7Unapokuwa sasa mabomoko matupu,

Yerusalema unakumbuka utukufu wake.

Ulipoangukia katika mikono ya waadui zake,

hakuna aliyekuwa pale kwa kuusaidia.

Washindi wake walichekelea kuanguka kwake.

8Muji Yerusalema ulitenda zambi kubwa,

ukakuwa muchafu kwa ajili ya zambi zake.

Wote waliousifia wanauzarau,

maana wameuona uchi wake.

Muji wenyewe unaugua na kujificha kwa ajili ya haya.

9Uchafu wake ulionekana waziwazi,

lakini muji wenyewe haukujali mwisho wake.

Anguko lake lilikuwa kubwa sana;

hakuna anayeweza kuufariji.

Unasema:

Angalia, ee Yawe, mateso yangu,

maana adui yangu ameshinda.

10Waadui wamenyoosha mikono yao,

wapate kukamata vitu vyake vyote vya bei kali.

Kweli umeona watu wa mataifa wakiingia ndani ya hekalu,

watu ambao Yawe aliwakataza

kuingia kati kusanyiko lake.

11Watu wa Yerusalema wote wanaugua, wakitafuta chakula;

wanatoa vitu vyao vya bei kali kwa kupata chakula,

kusudi wajirudishie nguvu zao.

Nao muji unalia,

Ee Yawe, uniangalie,

ona jinsi nilivyogeuka kuwa zaifu.

12Enyi wapita njia wote, hivi hamujali kitu?

Muangalie, muone kama kuna aliyepatwa na uchungu kama mimi,

uchungu Yawe alioniletea siku ya hasira yake kali.

13Aliteremusha moto kutoka juu,

ukanichoma hata ndani ya mifupa yangu.

Alinitegea wavu akaninasa,

kisha akanirudisha nyuma,

akaniacha peke yangu na kuzimia muchana kutwa.

14Aliyahesabu makosa yangu yote

akayakusanya pahali pamoja;

aliyafunga katika shingo langu kama nira,

nikafyonzwa nguvu zangu kwa uzito wake.

Yawe aliniweka katika mikono ya

watu ambao siwezi kuwapinga.

15Yawe aliwakataa waaskari walionilinda,

alitangaza wakati kamili wa kuniazibu

kuwaponda vijana wangu wanaume.

Aliwaponda kama katika kikamulio,

watu wangu wa Yuda.

16Kwa sababu ya hayo ninalia,

machozi yananitiririka,

sina mutu yeyote wa kunifariji;

hakuna yeyote wa kunitia moyo.

Watoto wangu wameachwa ukiwa,

maana adui yangu amenishinda.

17Ninainyoosha mikono yangu

lakini hakuna wa kunifariji.

Yawe ametoa amri juu yangu mimi Yakobo,

wajirani zangu wakuwe waadui zangu.

Kweli, mimi Yerusalema nimekuwa kitu kichafu kwao.

18Lakini Yawe amefanya sawa

kwa maana nimeliasi neno lake.

Munisikilize enyi watu wote,

muyaangalie mateso yangu.

Wabinti zangu na vijana wangu wanaume

wamepelekwa katika utumwa.

19Niliwaita wapenzi wangu,

lakini wao wakanidanganya.

Makuhani na wazee wangu wamekufia katika muji,

wakijitafutia chakula kusudi wajirudishie nguvu zao.

20Ona, ee Yawe, ninavyokuwa tabani.

Roho yangu imechafuka,

moyo wangu unaugua

maana nimekuasi vibaya.

Kule inje kumejaa mauaji,

ndani nako ni kama kifo tu.

21Sikiliza ninavyolalamika;

hakuna wa kunifariji.

Waadui zangu wote wamesikia juu ya taabu yangu:

wanafurahi kwamba umeniletea hasara.

Uifanye ile siku uliyoahidi ifike,

uwafanye nao wateseke kama mimi.

22Uwaazibu kwa ajili ya uovu wao wote.

Uwatendee kama ulivyonitendea mimi,

kwa sababu ya makosa yangu yote.

Ninaugua sana kwa maumivu

na moyo wangu unazimia.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help