1Ujumbe wa Mungu juu ya jangwa kando ya bahari.
Kama upepo mukali unaovuma kutoka kusini,
washambulizi wanakuja kutokea katika jangwa,
kutoka katika inchi ya kutisha.
2Nimeonyeshwa maono ya kutisha:
wadanganyifu wanadanganya na
waangamizaji wanaangamiza.
Mupande kwa kupigana vita, enyi Waelamu!
Mushambulie, enyi Wamedi!
Mungu atakomesha mateso yote
yaliyoletwa na Babeli.
3Kwa maono hayo nimeingiwa na woga mukubwa.
Maumivu mengi yamenishika,
kama maumivu ya mama anayezaa.
Nimefazaika zaidi hata siwezi kusikia;
nimefazaika hata siwezi kuona.
4Moyo unanidunda na woga umenishika.
Nilitamani magaribi ifike,
lakini ilipofika ikakuwa ya kutetemesha.
5Chakula kimetayarishwa,
mikeka zimetandikwa,
sasa watu wanakula na kunywa.
Kwa rafla, sauti inasikilika:
Musimame enyi watawala!
Muweke silaha tayari!
6Bwana aliniambia:
Kwenda uweke mulinzi;
umwambie atangaze atakachoona.
7Akiona kikundi, waaskari wapanda-farasi wawiliwawili,
wapanda-ngamia na wapanda-punda,
akuwe macho. Akuwe macho kabisa!
8Kisha, huyo mulinzi akalalamika:
Bwana, nimesimama juu ya munara wa ulinzi muchana kutwa,
nimeshika zamu usiku kucha!
9Angalia, wanakuja:
waaskari wapanda-farasi wawiliwawili.
Wanasema: Babeli umeanguka! Umeanguka!
Sanamu zote za miungu yake
zimetupwa chini na kuvunjwavunjwa!
10Ewe Israeli, watu wangu,
enyi muliotwangwa na kupepetwa kama ngano.
Sasa nimewaambia ninyi mambo niliyoyasikia
kwa Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli.
Ufunuo juu ya Edomu11Ujumbe wa Mungu juu ya Duma.
Ninasikia mutu ananiita kutoka Seiri:
Mulinzi, nini kipya leo usiku?
Kuna kipya chochote leo usiku?
12Nami mulinzi nikajibu:
Asubui inakuja, vilevile usiku;
ukitaka kuuliza, uliza tu;
kwenda urudi tena.
Ufunuo juu ya inchi ya Arabia13Ujumbe wa Mungu juu ya Arabia.
Enyi makundi ya wasafiri ya Dedani,
mupige kambi leo usiku katika pori za Arabia.
14Enyi wakaaji wa inchi ya Tema,
muwape maji hao wenye kiu;
muwapelekee chakula hao wakimbizi.
15Maana wamekimbia mapanga,
mapanga yaliyochomolewa,
pinde zilizovutwa na ukali wa mapigano.
16Maana Bwana aliniambia hivi: Katika muda wa mwaka mumoja, bila kuzidi wala kupunguka, utukufu wote wa Kedari utakwisha.
17Wapigapinde wachache kati ya mashujaa wa watu wa Kedari ndio watakaobaki. Ni Yawe, Mungu wa Israeli, anayesema hivyo.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.