1Afazali kula mukate wenye kukauka kwa amani kuliko karamu katika nyumba ya ugomvi.
2Mutumwa mwenye hekima atatwaa nafasi ya mwana mupumbafu. Atapata sehemu ya urizi wa jamaa hiyo.
3Zahabu na feza vinapimwa kwa moto, lakini Yawe ndiye anayepima mioyo ya watu.
4Mutenda maovu anasikiliza maneno mabaya; mwongo anategea sikio ulimi mudanganyifu.
5Anayechekelea masikini anamutukana Muumba wake; anayefurahia hasara hatakosa kuazibiwa.
6Taji la sifa la wazee ni wajukuu wao. Heshima ya wana ni baba yao.
7Maneno mazuri hayastahili katika kinywa cha mupumbafu, zaidi sana maneno ya uongo katika kinywa cha kiongozi!
8Kwa anayetoa kituliro ni kama hirizi; kila kitu anachofanya yeye anafanikiwa.
9Anayesamehe makosa anajenga urafiki, lakini anayekumbusha makosa anatenga warafiki.
10Onyo kwa mwenye akili lina maana, kuliko mapigo mia moja kwa mupumbafu.
11Nia ya mutu mwovu ni kuasi tu; mujumbe mubaya atatumwa juu yake.
12Afazali kukutana na dubu dike aliyenyanganywa watoto wake, kuliko kukutana na mupumbafu katika upumbafu wake.
13Mwenye kulipa mazuri kwa mabaya, mabaya hayataondoka katika nyumba yake.
14Kuanzisha ugomvi ni kama kufungua maji ya kisima; achana na ugomvi mbele haujafurika.
15Kumuhesabu mwovu kuwa na haki na kumwazibu asiyekuwa na kosa, yote mawili ni chukizo kwa Yawe.
16Kwa nini mupumbafu kuwa na feza katika mukono kwa kununua hekima, wakati yeye mwenyewe hana akili?
17Rafiki wa kweli ni rafiki siku zote. Ndugu anazaliwa kusudi asaidie wakati wa taabu.
18Mutu asiyekuwa na akili anajitoa rehani kwa deni ya mutu mwingine.
19Anayependa ugomvi anapenda zambi. Anayejivuna anajitafutia maangamizi.
20Mwenye moyo mupotovu hafanikiwi, na musema uongo anapatwa na hasara.
21Mutoto mupumbafu ni huzuni kwa baba yake, na baba wa mupumbafu hana furaha.
22Moyo wenye furaha ni dawa, lakini moyo wenye huzuni unakondesha mwili.
23Mutu mubaya anapokea kituliro kwa siri kusudi apate kupotosha haki.
24Hekima ni mbele ya uso wa mwenye akili, lakini macho ya mupumbafu yanaangalia kwa miisho ya dunia.
25Mutoto mupumbafu ni huzuni kwa baba yake, na uchungu kwa mama yake muzazi.
26Si vizuri kumwazibu mutu asiyekuwa na kosa; ni kosa kuwapiga fimbo wenye heshima.
27Asiyesema sana ana maarifa; mutu mutulivu ni mwenye ufahamu.
28Hata mupumbafu akinyamaza, anaonekana kuwa na hekima; akifunga kinywa chake anaonekana kuwa mwenye akili.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.