Wagalatia 1 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Salamu

1-2Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo na kwa wandugu wote wanaokuwa pamoja nami. Ni mimi niliyeitwa kuwa mutume, si kwa kuchaguliwa na watu, wala kwa njia ya mutu, lakini kwa njia ya Yesu Kristo na ya Mungu Baba aliyemufufua. Tunawaandikia ninyi makanisa ya Galatia.

3Tunawatakia neema na amani kutoka kwa Mungu Baba na kwa Bwana wetu Yesu Kristo.

4Kristo alijitoa mwenyewe kwa kutuokoa toka katika zambi zetu, kusudi atukomboe katika dunia hii mbaya ya sasa, kwa mapenzi ya Mungu Baba yetu.

5Mungu atukuzwe kwa milele na milele! Amina.

Habari Njema ni moja

6Ninashangaa sana kuona namna gani munageuka hivi upesi kwa kumwacha yule aliyewaita kwa njia ya neema ya Kristo na kufuata habari njema ya namna ingine.

7Kwa kweli hakuna Habari Njema ingine, lakini kuko watu wanaowavuruga, wakitaka kugeuza Habari Njema ya Kristo.

8Lakini kama sisi wenyewe au malaika kutoka mbinguni, akiwahubiri ninyi Habari Njema inayokuwa mbalimbali na ile tuliyowahubiri, alaaniwe!

9Tumekwisha kuwaambia mambo haya zamani, nami ninayarudilia tena: mutu akiwahubiri habari njema inayokuwa mbalimbali na ile muliyopokea, alaaniwe!

10Basi kusema vile inaonyesha kwamba ninatafuta watu wanikubali? Hapana! Ninataka kukubaliwa na Mungu. Au ninatafuta kuwapendeza watu? Kama ningekuwa ningali ninatafuta kuwapendeza watu, singekuwa mutumishi wa Kristo.

Kuitwa kwa Paulo

11Wandugu zangu, ninawajulisha kwamba Habari Njema ninayohubiri haikutungwa na mutu.

12Sikuipokea kutoka kwa mutu wala sikuifundishwa na mutu, lakini ni Yesu Kristo aliyeifunua kwangu.

13Mumesikia namna mwenendo wangu ulivyokuwa zamani, wakati nilipofuata dini ya Kiyuda. Munajua namna nilivyotesa kanisa la Mungu vikali sana na kujikaza kwa kuliharibu.

14Nami niliendelea vizuri sana katika dini ya Kiyuda kuwapita watu wote wengine wa kabila langu wenye umri wangu, nikijikaza sana kushika desturi za babu zetu.

15Lakini, Mungu aliyenichagua mbele sijazaliwa na kuniita kwa neema yake, alipendezwa

16kumufunua Mwana wake kwangu, kusudi nihubiri Habari yake Njema kwa watu wa mataifa mengine. Na pale pale sikuomba shauri kwa mutu yeyote,

17wala sikwenda Yerusalema kwa kuonana na wale waliokuwa mitume mbele yangu, lakini nikajiendea katika inchi ya Arabia. Kisha nikarudia tena Damasiki.

18Kulipokwisha kupita miaka mitatu, nikaenda Yerusalema kusudi nipate kujuana na Petro, nami nikakaa kwake kwa muda wa siku kumi na tano.

19Sikumwona mutu mwingine isipokuwa tu Yakobo, ndugu ya Bwana.

20Ninaapa mbele ya Mungu kuwa sisemi uongo katika maneno haya ninayowaandikia.

21Nyuma ya pale nikaenda pande za jimbo la Suria na la Kilikia.

22Katika siku zile makanisa ya Yudea yalikuwa hayajaniona kwa uso,

23lakini yalikuwa yakisikia tu habari kwamba: “Yule aliyekuwa akitutesa zamani, sasa anahubiri habari za imani ile aliyokuwa akipotosha.”

24Nao yalimusifu Mungu kwa ajili yangu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help