1Yawe akasema na Musa, akamwambia:
2Uwalipize kisasi Wamidiani mambo waliyowatendea Waisraeli; kisha wewe utakufa.
3Basi Musa akazungumuza na watu akawaambia: Mutayarishe watu kwa vita waende kuwashambulia Wamidiani kwa kumulipizia Yawe kisasi.
4Kutoka kila kabila la Israeli, mutapeleka watu elfu moja kwa vita.
5Basi, watu elfu moja walitolewa kutoka kila kabila kati ya maelfu ya Waisraeli, jumla wanaume elfu kumi na mbili wenye silaha.
6Musa akawapeleka kwa vita chini ya uongozi wa Finehasi mwana wa kuhani Eleazari, akiwa na vyombo vya Pahali Patakatifu na baragumu za kutoa kitambulisho.
7Wakashambulia inchi ya Midiani, kama vile Yawe alivyomwamuru Musa, wakawaua wanaume wote.
8Kati ya watu hao waliouawa, kulikuwa wafalme watano wa Midiani: Ewi, Rekemu, Suri, Huri na Reba. Vilevile wakamwua Balamu mwana wa Beori.
9Waisraeli wakawapeleka kuwa wafungwa wanawake wa Midiani na watoto wao. Wakanyanganya: ngombe, kondoo na mali yao yote.
10Miji yao yote, makao yao na kambi zao zote wakaziteketeza kwa moto.
11Wakabeba vitu vyote walivyonyanganya na vile vyote walivyoteka na watu na ya nyama,
12wakamupelekea Musa na Eleazari, na Waisraeli wote waliokuwa katika kambi katika inchi za mabonde za Moabu, ngambo ya Yordani karibu na Yeriko.
Kurudi toka kwa vita13Musa, kuhani Eleazari, na viongozi wote wa Waisraeli wakatoka katika kambi, wakaenda kupokea waaskari.
14Musa akakasirikishwa na wakubwa wa jeshi na majemadari waliosimamia makundi ya waaskari elfu na makundi ya waaskari mamia waliorudi kutoka katika vita.
15Musa akawauliza: Kwa nini mumewaacha wanawake hawa wote wazima?
16Mukumbuke kwamba wanawake ndio waliofuata shauri la Balamu, wakasababisha Waisraeli wamwasi Yawe kule Peori hata ugonjwa mukali ukawafikia watu wa Yawe. Ang. Hes 25.1-9
17Kwa hiyo basi, muwaue hawa watoto wote wanaume na kila mwanamuke kati yao aliyekwisha kulala na mwanaume.
18Lakini musiwaue wabinti wote ambao hawajapata kulala na mwanaume; muwaache wazima kwa ajili yenu wenyewe.
19Wote wale wanaokuwa kati yenu ambao wameua mutu au kugusa maiti wanapaswa kukaa inje ya kambi kwa muda wa siku saba; mujitakase pamoja na mateka wenu katika siku ya tatu na ya saba.
20Munapaswa kutakasa vilevile kila nguo, kila kitu kilichotengenezwa kwa ngozi, kwa manyoya ya kondoo au kwa muti.
21Kuhani Eleazari akawaambia wanaume waliorudi toka kwa vita: Hii ndiyo sheria ambayo Yawe amemupa Musa.
22Zahabu, feza, shaba, chuma, manjanja na madini ya risasi,
23ni kusema vitu vyote ambavyo vinavyovumilia moto, vitatakaswa kwa kupitishwa ndani ya moto. Hata hivyo, vinapaswa kutakaswa kwa maji ya utakaso. Vitu vingine vyote ambavyo haviwezi kuvumilia moto vitatakaswa kwa maji ya utakaso.
24Siku ya saba munapaswa kufua nguo zenu; ndipo mutakapokuwa safi na kuruhusiwa kuingia katika kambi.
Kugawanywa kwa vitu vilivyonyanganywa25Yawe akasema na Musa, akamwambia:
26Wewe na kuhani Eleazari, pamoja na viongozi wa ukoo wa Waisraeli, mufanye hesabu ya vitu vilivyonyanganywa, watu na nyama.
27Mugawanye vitu katika mafungu mawili, fungu moja la waaskari waliokwenda kwa vita na fungu lingine kwa ajili ya watu wote wengine.
28Kisha kutokana na lile fungu la waaskari waliokwenda kwa vita, tenga sehemu ya kumi kwa ajili ya Yawe: kitu kimoja kutoka kila vitu mia tano, ikuwe ni watu, ngombe, punda, kondoo au mbuzi,
29umupe kuhani Eleazari kuwa sadaka kwa Yawe.
30Kutoka katika lile fungu la jamii nzima, utwae mumoja kati ya kila makumi tano, ikuwe ni watu, ngombe, punda, kondoo na mbuzi. Hivyo utawapa Walawi ambao wanashugulika na kazi katika hema la Yawe.
31Musa na kuhani Eleazari wakafanya kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.
32Vitu watu waliotoka kwa vita walivyonyanganya vilikuwa: kondoo elfu mia sita na makumi saba na tano,
33ngombe elfu makumi saba na mbili,
34punda elfu makumi sita na moja,
35na wabinti elfu makumi tatu na mbili ambao hawakukuwa wamelala na mwanaume.
36Nusu yake, sehemu ambayo iligawanyiwa kwa waaskari waliokwenda kwa vita, ilikuwa kondoo elfu mia tatu makumi tatu na saba na mia tano,
37katika hao mia sita makumi saba na watano walitolewa kwa Yawe.
38Ngombe wa waaskari walikuwa elfu makumi tatu na sita, na katika hao makumi saba na wawili walitolewa sehemu ya kumi kwa Yawe.
39Punda wao walikuwa elfu makumi tatu mia tano, na katika hao makumi sita na mumoja walitolewa sehemu ya kumi kwa Yawe.
40Watu walikuwa elfu kumi na sita, na katika hao sehemu ya Yawe ilikuwa ni watu makumi tatu na wawili.
41Basi, Musa akamupa kuhani Eleazari sehemu ya kumi hiyo iliyotolewa kwa Yawe, kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.
42Ile nusu Waisraeli waliyopewa, ambayo Musa alitenga na ile nusu waaskari waliokwenda kwa vita waliyopewa,
43ilikuwa kondoo elfu mia tatu na makumi tatu na saba na mia tano,
44ngombe elfu makumi tatu na sita,
45punda elfu makumi tatu na mia tano,
46na watu elfu kumi na sita.
47Kutoka nusu hii Waisraeli waliyopewa, Musa alitwaa mumoja kati ya kila mateka makumi tano na nyama makumi tano, kama alivyoamriwa na Yawe, akawapa Walawi ambao walitumika katika hema la Yawe.
48Kisha wakubwa wa majeshi, makapiteni na majemadari wa jeshi wakamwendea Musa
49wakamwambia: Sisi watumishi wako tumewahesabu waaskari wote wanaokuwa chini yetu na tumeona kwamba hakuna hata mumoja wao anayekosekana.
50Basi, tumeleta vyombo vya zahabu, mikufu, vikomo, pete za muhuri, pete za masikio na ushanga ambavyo kila mutu alipata. Tumevitoa kusudi nafsi zetu zifanyiwe upatanisho mbele ya Yawe.
51Musa na kuhani Eleazari wakapokea vitu vyote vilivyopambwa kwa zahabu.
52Jumla ya zahabu yote waliyomutolea Yawe ilikuwa karibu kilo mia mbili.
53(Kila askari alijitwalia vitu vyake mwenyewe).
54Basi, Musa na kuhani Eleazari wakapokea zahabu hiyo kutoka kwa majemadari wakaipeleka katika hema la mukutano, ikuwe ukumbusho wa Waisraeli mbele ya Yawe.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.