Kumbukumbu la Sheria 25 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1“Ikiwa kuna ugomvi kati ya watu wawili, na wakienda kwa tribinali kuamua maneno yao, mumoja akionekana hana kosa, na mwingine akihukumiwa,

2kama yule aliyehukumiwa amepewa azabu ya kupigwa fimbo, mwamuzi atamwamuru huyo alale chini na kupigwa fimbo kulingana na kosa lake.

3Mwenye kosa anaweza kupigwa fimbo makumi ine lakini si zaidi. Mukizidisha kiasi hicho mutakuwa mumemufezehesha ndugu yenu.

4“Usimufunge ngombe kinywa anapopepeta ngano.

Madaraka juu ya kaka na ndugu marehemu

5“Kama wandugu wanaishi pahali fulani na mumoja wao akikufa bila kuacha mutoto mwanaume, muke wa marehemu asiolewe na mutu mwingine inje ya jamaa hiyo. Yule ndugu wa marehemu anapaswa kumwoa mujane huyo.

6Mutoto wa kwanza mwanaume atakayezaliwa nao atahesabiwa kuwa wa marehemu kusudi jina lake lisifutwe katika inchi ya Israeli.

7Lakini kama huyo ndugu wa marehemu hamutaki huyo mwanamuke mujane, basi, mwanamuke huyo atakwenda mbele ya wazee wa muji na kusema: ‘Kaka wa mume wangu marehemu anakataa kuendelesha jina la kaka yake marehemu katika Israeli; hapendi kunitimizia madaraka yake ya kaka wa mume wangu marehemu’.

8Kisha wazee wa muji watamwita huyo mwanaume na kuongea naye. Kama ataendelea kukataa kwamba hataki kumwoa,

9huyo mwanamuke mujane atamwendea mbele ya hao wazee wa muji, atamuvua kiatu chake kimoja na kumutemea mate kwenye uso na kumwambia: ‘Hivi ndivyo anavyopaswa kutendewa mutu anayekataa kudumisha nyumba ya kaka yake’.

10Na jina la nyumba yake katika Israeli litakuwa: ‘Nyumba ya mutu aliyevuliwa kiatu.’ ”

Sheria zingine

11“Wanaume wawili wakipigana na muke wa mumoja wao akimusaidia mume wake kwa kumukamata sehemu za siri yule anayepigana na mume wake,

12mutakata mukono wa kuume wa yule mwanamuke; musimuhurumie.

13“Musikuwe na vipimo vya kupimia vya namna mbili: kimoja kizito na kingine chepesi. Musitumie mizani za udanganyifu.

14Wala musikuwe na aina mbili za vipimo vya kupimia, kubwa na ndogo.

15“Mutumie mizani na vipimo vyenye uzito kamili na vya haki mupate kuishi maisha marefu katika inchi Yawe, Mungu wenu, anayowapa.

16Wote wanaofanya mambo hayo, wote wanaotenda kwa udanganyifu ni chukizo kwa Yawe, Mungu wenu.

Amri ya kuwaua Waamaleki

17“Mukumbuke kitendo cha Waamaleki mulipokuwa katika safari kutoka Misri.

18Mukumbuke jinsi walivyowashambulia huko katika njia mukiwa wazaifu na kuwapiga wale wote waliokuja nyuma yenu wamechoka. Waamaleki hawakumwogopa Mungu.

19Kwa hiyo wakati Yawe, Mungu wenu, atakapowapumzisha kutokana na mashambulio ya waadui zenu wote wanaowazunguka katika inchi ambayo amewapa kuwa urizi wenu na kuishi humo, munapaswa kuangamiza Waamaleki wote.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help