1Yawe akamwambia Musa:
2Uwaambie Waisraeli hivi: Katika sikukuu zangu mimi Yawe ambazo zimepangwa mutakuwa na mukutano mutakatifu. Sikukuu ambazo nimepanga ni hizi:
3Kutakuwa siku sita za kufanya kazi. Lakini siku ya saba ni Sabato. Siku hiyo ni ya mapumziko, hamutafanya kazi na mutakuwa na mukutano mutakatifu. Siku hiyo ya saba hamutafanya kazi. Hiyo ni Sabato ambayo ni takatifu kwangu mimi Yawe katika makao yenu yote.
4Sikukuu zingine zangu mimi Yawe ambazo mutakuwa na mukutano mutakatifu zitafanyika katika wakati huu uliopangwa.
Sikukuu ya Pasaka(Hes 28.16-25)5Magaribi ya siku ya kumi na ine ya mwezi wa kwanza mutafanya kwa heshima yangu mimi Yawe sikukuu ya Pasaka. Sikukuu ya mwaka mupya(Hes 29.1-6)
23Yawe akamwambia Musa:
24Uwaambie watu wa Israeli hivi: Siku ya kwanza ya mwezi wa saba mutafanya siku ya mapumziko, siku ya ukumbusho itakayotangazwa kwa mulio wa baragumu na kufanya mukutano mutakatifu.
25Musifanye kazi siku hiyo na munitolee mimi Yawe sadaka ya kuteketezwa kwa moto.
Siku ya upantanisho(Hes 29.7-11)26Yawe akamwambia Musa: Ang. Law 16.29-34
27Siku ya kumi ya mwezi huu wa saba ni siku ya upatanisho. Siku hiyo ni siku ya kuwa na mukutano mutakatifu. Mutafunga kula na kutoa sadaka Yawe anazotolewa kwa moto.
28Musifanye kazi zenu zozote za kawaida siku hiyo. Siku hiyo ni siku ya upatanisho, siku ya kuwafanyia ninyi upatanisho mbele ya Yawe, Mungu wenu.
29Mutu yeyote asiyefunga kula siku hiyo ni lazima atengwe mbali na watu wake.
30Mutu yeyote atakayefanya kazi yoyote siku hiyo nitamwangamiza kutoka watu wake.
31Musifanye kazi: hili ni sharti la kufuata siku zote katika vizazi vyenu, na katika makao yenu yote.
32Siku hiyo, itakuwa kwenu Sabato ya mapumziko na mutafunga. Siku ya Sabato ni siku ya kumi ya mwezi huo tangu magaribi mpaka magaribi inayofuata.
Sikukuu ya vibanda(Hes 29.12-39; Kumb 16.13-17)33Yawe akamwambia Musa: Ang. Kumb 16.13-15
34Uwaambie Waisraeli hivi: Tangu siku ya kumi na tano ya mwezi huo wa saba mutafanya sikukuu ya vibanda kwa muda wa siku saba kwa heshima ya Yawe.
35Siku ya kwanza ya siku hizo saba, mutakuwa na mukutano mutakatifu na musifanye kazi.
36Kwa muda wa siku saba mutatoa sadaka Yawe anazopewa kwa moto. Siku ya nane mutakuwa na mukutano mutakatifu na kumutolea Yawe sadaka ya kuteketezwa. Mukutano huo ni mutakatifu. Siku hiyo musifanye kazi.
37Hizo ndizo sikukuu za Yawe zilizopangwa ambazo mutatoa tangazo kuwe mukutano mutakatifu wa kumutolea Yawe sadaka zinazotolewa kwa moto, sadaka za kuteketezwa na sadaka za vyakula, matoleo na sadaka za kinywaji, kila moja kwa siku yake yenyewe.
38Sadaka hizo ni pamoja na zile munazonitolea mimi Yawe siku ya Sabato kama vile na sadaka zenu za kawaida, sadaka za kutimiza viapo vyenu, na sadaka zenu za mapenzi munazonitolea mimi Yawe.
39Kisha kuvuna mashamba yenu mutafanya sikukuu kwa muda wa siku saba, tangu siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba. Siku ya kwanza itakuwa siku ya mapumziko na hata siku ya nane.
40Katika siku ya kwanza mutatwaa matunda ya miti yenu mizuri, matawi ya ngazi, matawi yenye majani mengi na matawi ya miti inayoota kandokando ya muto, nanyi mutafanya sikukuu mbele ya Yawe, Mungu wenu kwa siku saba.
41Kila mwaka munapaswa kufanya sikukuu hii kwa muda wa siku saba kwa heshima ya Yawe. Hili ni sharti la kufuata siku zote katika vizazi vyenu. Mutaifanya katika mwezi wa saba.
42Kwa muda wa siku saba mutaishi katika vibanda. Wakaaji wote wa Israeli wataishi katika vibanda wakati huo.
43Jambo hilo litajulisha vizazi vyenu kwamba nilipowatoa babu zenu katika inchi ya Misri, niliwafanya waishi katika vibanda. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.
44Musa akawatangazia Waisraeli sikukuu za Yawe zilizopangwa.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.