2 Mambo ya Siku 21 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Yosafati akakufa na kuzikwa pamoja na babu zake katika makaburi ya kifalme katika muji wa Daudi; naye Yoramu mwana wake akatawala pahali pake.

Mufalme Yoramu wa Yuda(2 Sik 8.17-24)

2Yoramu alikuwa na wandugu, wana wa Yosafati; Azaria, Yehieli, Zakaria, Azaria, Mikaeli na Sefatia.

3Baba yao aliwapa zawadi kubwakubwa za feza, zahabu na vitu vingine vya bei kali, na vilevile miji ya Yuda yenye kuta. Lakini kwa sababu Yoramu ndiye aliyekuwa muzaliwa wake wa kwanza, Yosafati akamupa ufalme atawale kwa pahali pake.

4Yoramu alipoikalia kiti cha kifalme na utawala wake ulipokuwa umekwisha kuimarika, yeye akawaua wandugu zake wote kwa upanga, na vilevile wakubwa wamoja wa Israeli.

5Yoramu alianza kutawala akiwa na umri wa miaka makumi tatu na miwili. Alitawala akiwa kule Yerusalema kwa muda wa miaka minane.

6Alifuata njia mbaya za mufalme Ahabu na za wafalme wengine wa Israeli kama vile jamaa ya Ahabu ilivyofanya kwa sababu muke wake alikuwa binti ya Ahabu. Akatenda maovu mbele za Yawe,

7lakini Yawe hakutaka kuangamiza ukoo wa Daudi kwa ajili ya agano alilokuwa amefanya na Daudi vilevile kwa sababu alikuwa ameahidi kwamba wazao wake wataendelea kutawala milele.

8Wakati wa utawala wa Yoramu, Waedomu waliasi utawala wa Yuda, wakaweka mufalme wao wenyewe. Ang. Mwa 27.40

9Kwa hiyo, Yoramu pamoja na wakubwa wake na magari yake yote akaondoka akawashambulia Waedomu waliokuwa wamemuzunguka yeye pamoja na wakubwa wake na magari.

10Hivyo Waedomu wakaasi utawala wa Yuda mpaka sasa. Wakati uleule, vilevile wakaaji wa Libuna nao wakaasi utawala wake kwa sababu Yoramu alikuwa amemwacha Yawe, Mungu wa babu zake.

11Tena alitengeneza pahali pa kuabudia miungu mingine katika milima ya Yuda na kusababisha wakaaji wa Yerusalema kukosa uaminifu na watu wa Yuda kupotoka.

12Nabii Elia akamupelekea mufalme Yoramu barua hii:

“Yawe, Mungu wa Daudi babu yako, anakulaani kwa sababu haukufuata mwenendo wa Yosafati baba yako, au wa Asa mufalme wa Yuda.

13Lakini umeifuata mienendo ya wafalme wa Israeli na kuwaongoza watu wa Yuda na wa Yerusalema katika kukosa uaminifu kama vile Ahabu, na wafalme wa jamaa yake waliomufuata walivyoongoza Israeli kukosa uaminifu. Vilevile umewaua wandugu zako, wandugu za baba mumoja waliokuwa watu wema zaidi kuliko wewe.

14Kwa sababu hiyo, Yawe atawaazibu vikali watu wako, wana wako, wake zako na kuharibu mali yako yote.

15Wewe mwenyewe utapata ugonjwa mukali wa tumbo, ambao utaongezeka siku kwa siku, mpaka matumbotumbo yako yatoke inje.”

16Kulikuwa Wafilistini na Waarabu wengine waliokuwa wakikaa karibu na Waetiopia. Hawa, Yawe aliwapandisha hasira kusudi wapigane vita na Yoramu.

17Basi, wakashambulia inchi ya Yuda, wakanyanganya mali yote iliyokuwa katika nyumba yake na kutwaa wana wake wote na wake zake, isipokuwa Ahazia, mwana wake mudogo.

18Nyuma ya hayo yote, Yawe akamuletea mufalme ugonjwa wa tumbo usioweza kupona.

19Aliendelea kugonjwa, na ugonjwa wake ukakuwa unaongezeka siku kwa siku, hata kufikia mwisho wa mwaka wa pili, akakufa katika maumivu makali. Watu hawakuwasha moto kwa kuomboleza kifo chake kama vile walivyowafanyia babu zake.

20Yoramu alianza kutawala akiwa na umri wa miaka makumi tatu na miwili; akatawala kule Yerusalema kwa muda wa miaka minane. Wakati alipokufa, hakuna mutu yeyote aliyemusikitikia. Alizikwa katika muji wa Daudi, lakini si katika makaburi ya wafalme.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help