1Maisha yenu katika kuungana kwenu na Kristo si yanawatia ninyi nguvu? Nao upendo wake si unawafariji ninyi? Si munaishi katika ushirika na Roho Mutakatifu? Si muko na moyo mwema na wa huruma?
2Basi munijaze na furaha tele, mukiwa na nia moja, na upendo mumoja, roho moja na wazo moja.
3Musifanye jambo lolote kwa roho ya mapingano wala kwa kujivuna bure, lakini munyenyekeane kila mutu akimuhesabu mwenzake kuwa muzuri kuliko yeye mwenyewe.
4Kila mutu asitafute faida yake mwenyewe, lakini atafute faida ya watu wengine.
5Ndani yenu mukuwe na nia kama hii iliyokuwa ndani ya Kristo Yesu:
6Tangu mwanzo yeye alikuwa na hali ya Mungu,
lakini hakuona kwamba kuwa sawa na Mungu ni kitu cha kushikamana nacho.
7Alitupilia hivi vyote, akatwaa hali ya mutumwa.
Akatwaa mufano wa mutu, naye akaonekana katika hali ya kimutu.
8Alijinyenyekeza na kutii mpaka kufa, ndiko kufa kwake juu ya musalaba.
9Kwa hiyo Mungu naye akamwinua juu zaidi, akamupa jina lenye ukubwa kuliko majina yote,
10kusudi kwa kuheshimu jina la Yesu, viumbe vyote vinavyokuwa katika mbingu, katika dunia na katika kuzimu, vipige magoti mbele yake,
11na kila mutu akubali kwamba Yesu ni Bwana, naye Mungu Baba atatukuzwa kwa njia hiyo.
Kuwa kama mwangaza katika dunia12Basi wapendwa wangu, mulionyesha utii wenu siku zote wakati nilipokuwa kwenu, na sasa ingekuwa vema muendelee kufanya vile katika siku hizi ninapokuwa mbali nanyi. Mutumike kwa ajili ya wokovu wenu kwa woga na kutetemeka,
13kwa maana Mungu anafanya kazi ndani yenu na kuwapa moyo wa kutaka na kutimiza mambo yanayolingana na mupango wake mwema.
14Mufanye kila kitu bila manunguniko wala mabishano,
15kusudi mupate kuwa bila kosa na kuwa na maisha safi. Hivi mutakuwa watoto wakamilifu wa Mungu wasiokuwa na kilema kati ya watu waovu na wapotovu wa dunia hii. Munapaswa kuangaza kati ya watu hawa kama vile nyota zinavyoangaza katika mbingu,
16mukiwatangazia habari inayoleta uzima. Hivi nitapata sababu ya kujivuna Siku ile ya kurudia kwa Kristo kwa maana itakuwa kitambulisho cha kuhakikisha kwamba bidii yangu na kazi yangu havikupotea bure.
17Hata nikitoa maisha yangu kuwa sadaka pamoja na imani yenu inayokuwa sadaka mbele ya Mungu, mimi ninafurahi na kushiriki pamoja nanyi wote.
18Nanyi vilevile mufurahi na kushiriki pamoja nami katika furaha yenu.
Timoteo na Epafrodito19Kama Bwana Yesu akitaka, ninangojea kisha muda kidogo kuwatumia Timoteo, kusudi nipate kutiwa moyo na habari nitakazopata kutoka kwenu.
20Ni yeye tu ndiye mafikiri yake yanapatana na yangu, naye anashugulika kweli na mambo yanayowaelekea.
21Watu wengine wote wanatafuta faida yao wenyewe, lakini hawashuguliki na Yesu Kristo.
22Munajua ninyi wenyewe namna Timoteo alivyojionyesha kwamba anastahili, kwa maana alitumika kazi ya kueleza Habari Njema pamoja nami kama vile mwana anavyotumika na baba yake.
23Ninatumaini kumutuma kwenu pale pale nitakapojua yale yatakayonitokea juu ya kufungwa kwangu.
24Nami ninamutumainia Bwana kwamba mimi mwenyewe nitakuja kuwaona bado kidogo.
25Niliona vema kuwatumia ndugu yetu Epafrodito, anayeshiriki pamoja nami katika kazi na katika vita ya Habari Njema. Ni yeye ndiye muliyetumia kwa kunisaidia kufuatana na mahitaji niliyokuwa nayo.
26Yeye yuko na hamu sana kuwaona ninyi wote, naye anahuzunika sana kwa sababu mulisikia kwamba alikuwa mugonjwa.
27Alikuwa mugonjwa karibu kufa, lakini Mungu akamuhurumia, na si yeye peke yake, lakini mimi vilevile kusudi nisikuwe na huzuni juu ya ingine.
28Hivi ninamutuma kwenu kwa haraka kusudi mupate kufurahi wakati mutakapomwona tena na huzuni yangu ipate kupunguka.
29Basi mumupokee kwa furaha kubwa sana kwa jina la Bwana. Munapaswa kuwapa watu wa namna hii heshima,
30kwa sababu yeye alikuwa karibu kufa kwa ajili ya kazi ya Kristo. Alihatarisha maisha yake kwa kuja kuniletea musaada ule ambao ninyi wenyewe musingeweza kunipatia.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.