1Ee Yawe,
mbona unasimama mbali?
Kwa nini unajificha wakati tuko katika taabu?
2Waovu wanatesa wamasikini kwa kiburi.
Mitego yao iwanase wao wenyewe!
3Mwovu anajisifia tamaa zake mbaya,
anapata faida kwa njia mbaya,
anazarau na kumukataa Yawe.
4Katika majivuno yake anasema: “Mungu hatagundua.
Hakuna Mungu.”
Hayo ndiyo mawazo yake yote.
5Njia za mwovu zinafanikiwa siku zote;
hukumu zako ziko mbali na mawazo yake,
na anazarau waadui zake wote.
6Anawaza ndani ya moyo: “Sitakuwa na wasiwasi;
sitapatwa na taabu katika maisha.”
7Kinywa chake kimejaa laana, udanganyifu na ukorofi;
ni mwepesi kusema maneno ya kuchukiza na maovu.
8Anajificha karibu na vijiji akivizia,
amwue kwa siri mutu asiyekuwa na kosa.
Yuko macho kumuvizia muzaifu;
9anajificha katika maficho yake kama simba.
Anavizia apate kuwakamata wamasikini;
anawanasa kwa mutego wake na kuwachukua.
10Muzaifu anashambuliwa na kuangushwa chini;
anaangushwa kwa ukali wa mutu mwovu.
11Mwovu anawaza ndani ya moyo wake: “Mungu amesahau;
ameficha uso wake, haoni kitu!”
12Ee Yawe,
simama sasa uwaazibu!
Usiwasahau wanaoteswa.
13Ee Mungu, kwa nini mwovu anakuzarau,
na kusema kwamba wewe haujali kitu?
14Lakini wewe unawaona wenye taabu na shida;
nawe uko tayari kuwasaidia siku zote.
Muzaifu anakutegemea wewe, ee Mungu,
wewe umekuwa siku zote musaada wa yatima.
15Uvunje nguvu za mutu mwovu;
ukomeshe uovu wake wote, usikuwe tena.
16Yawe ni mufalme milele na milele!
Mataifa yatatoweka katika inchi yake.
17Ee Yawe, unapokea maombi ya muzaifu;
unamutia moyo na kumutegea sikio.
18Utawatendea haki wayatima na wanaoteswa,
mwanadamu anayekuwa mavumbi asiweze tena kuleta hofu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.