1Usimukaripie muzee kwa nguvu, lakini umwonye kama baba yako. Uwatendee vijana wanaume kama wandugu zako,
2nao wanawake wazee kama mama yako na vijana wanawake kama wadada zako, ukijilinda katika maisha safi.
3Uwaheshimu wanawake wajane wasiokuwa na tegemeo lolote.
4Lakini kama mujane akiwa na watoto au wajukuu, inafaa wajifunze kwanza kutimiza mapaswa yao ya kidini kwa ajili ya jamaa zao wenyewe na kuwarudishia wazazi na babu zao mema waliyowatendea, kwa maana jambo hilo linamupendeza Mungu.
5Mujane wa kweli asiyekuwa na mutu yeyote wa kumusaidia, anamutumainia Mungu, na kudumu kumutolea mahitaji yake na kumwomba muchana na usiku.
6Lakini mujane anayeishi katika tamaa mbaya amekwisha kufa, ijapokuwa angali bado muzima.
7Hayo ndiyo maneno unayopaswa kuwaagiza wajane kusudi wasikuwe na mashitaki.
8Kama mutu asipotunza wandugu zake na hasa zaidi watu wa jamaa yake mwenyewe, huyu amekana imani yake naye ni mubaya kuliko mupagani.
9Usimwandike katika hesabu ya wajane mujane yeyote ambaye hajatimiza umri wa miaka makumi sita. Tena inafaa akuwe yule aliyeolewa na mume mumoja tu.
10Sherti ajulikane kwa matendo yake mema. Anapaswa kuwa mutu aliyeadibisha watoto wake vizuri, aliyekaribisha wageni, aliyewapokea watu wa Mungu akiwanawisha miguu, aliyewasaidia wenye taabu na aliyejitolea kwa kutenda mema ya kila namna.
11Lakini ukatae kuandika wajane wanaokuwa wangali vijana katika hesabu ile kwa maana wanapovutwa na tamaa ya kutaka kuolewa, wanaacha kumutumikia Kristo.
12Na kwa hiyo wanavunja agano walilofanya naye kwanza na kuanguka katika kosa.
13Na zaidi ya hiyo, wanashikwa na uvivu na kuwa na tabia ya kutangatanga nyumba kwa nyumba. Na si ile tu, vilevile wao ni wakatetea na wenye kujiingiza katika maneno ya watu wengine na kusema maneno yasiyofaa.
14Kwa sababu hiyo, ninataka wajane wanaokuwa wangali vijana waolewe, wazae watoto na kutunza nyumba zao, kusudi waadui wasipate nafasi ya kutuchongea.
15Kwa maana wajane wamoja wamekwisha kupotoka na kumufuata Shetani.
16Lakini kama mwamini yeyote akiwa na wajane katika jamaa lake, anapaswa kuwasaidia kusudi kanisa lisilemewe. Na hivi kanisa nalo litaweza kuwasaidia wale wajane wasiokuwa na tegemeo lolote.
17Wazee wa kanisa wanaoongoza kazi yao vizuri wanastahili kupokea mushahara mara mbili, hasa zaidi wale wanaojitolea kwa kufanya kazi ya kuhubiri na kufundisha.
18Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Usifunge kinywa cha ngombe anapokanyaga ngano.” Na tena yanasema: “Mutumishi anastahili kupewa mushahara wake.”
19Ukatae mashitaki juu ya muzee isipokuwa kwa ushuhuda wa watu wawili au watatu.
20Wale wenye kufanya zambi, uwakaripie mbele ya watu kusudi wengine wapate kuogopa vilevile.
21Ninakuagiza mbele ya Mungu na mbele ya Kristo Yesu na ya wamalaika watakatifu, ushike kanuni hizo bila kuwazia mutu kitu wala kuwa na upendeleo katika mambo yote unayofanya.
22Usiweke mikono juu ya mutu kwa haraka, wala usishiriki zambi za watu wengine. Ujilinde wewe mwenyewe katika maisha safi.
23Kwa ajili ya maumivu ya tumbo lako na uzaifu wa mwili wako wa kila mara, tangu sasa usikunywe maji tu, lakini utumie divai kidogo.
24Zambi za watu wamoja zinaonekana waziwazi hata mbele hawajahukumiwa. Lakini zambi za wengine zinajulikana kisha.
25Na ni hivi vilevile, matendo mazuri yanaonekana waziwazi, na hata yale yasiyoonekana wazi hayawezi kufichwa.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.