1Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi alipojifanya mwenda-wazimu mbele ya mufalme Abimeleki naye akamufukuza na Daudi akajiendea.
2Nitamutukuza Yawe nyakati zote,
sitaacha hata kidogo kutaja sifa zake.
3Mimi nitajisifu kwa ajili ya Yawe;
wanyenyekevu wasikie na kufurahi.
4Mumutukuze Yawe pamoja nami,
wote pamoja tulisifu jina lake.
5Nilimwomba Yawe, naye akanijibu,
na kuniondoa katika hofu zangu zote.
6Mumugeukie Mungu mupate kufurahi;
nanyi hamutafezeheka hata kidogo.
7Masikini alimulilia Yawe, naye akamusikia,
na kumwokoa katika taabu zake zote.
8Malaika wa Yawe anawalinda wote wanaomwabudu,
na kuwaokoa kutoka katika hatari.
9Mupime muone jinsi Yawe ni muzuri.
Heri mutu anayekimbilia kwake.
10Mumwabudu Yawe, enyi watakatifu wake,
maana wenye kumwabudu hawakosewi kitu.
11Hata simba wakali wanakosewa na kusikia njaa,
lakini wanaomutafuta Yawe hawakosewi chochote kizuri.
12Mukuje, enyi vijana munisikilize,
nami nitawafundisha kumwabudu Yawe.
13Unatamani kufurahia maisha,
kuishi maisha marefu na kufurahia mazuri?
14Basi, uache kusema mabaya,
na kuepuka kusema uongo.
15Ujiepushe na uovu, utende mazuri;
utafute amani na kuifuatilia.
16Yawe anawaangalia watu wa haki,
na kusikiliza malalamiko yao;
17lakini anawapinga watu wanaotenda maovu,
kusudi afute majina yao kutoka katika dunia.
18Watu wa haki wakimulilia Yawe, yeye anawasikia,
na kuwaokoa katika taabu zao zote.
19Yawe ni karibu na wenye kuvunjika moyo;
anawaokoa wote waliokata tamaa kabisa.
20Mateso ya mutu wa haki ni mengi,
lakini Yawe anamwokoa kutoka katika yote.
21Analinda viungo vya mwili wake wote,
hakuna hata mufupa wake mumoja utakaovunjwa.
22Ubaya unawaletea waovu kifo;
wanaowachukia watu wa haki wataazibiwa.
23Yawe anaokoa maisha ya watumishi wake,
wote wanaomukimbilia hawataazibiwa.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.