1Basi, Musa akawaambia Waisraeli kila kitu kama vile Yawe alivyomwamuru.
Maagizo juu ya viapo2Kisha Musa akazungumuza na viongozi wa makabila ya Israeli, akawaambia: Hili ndilo neno lililoamriwa na Yawe:
3Mutu akiahidi mbele ya Yawe au akifanya kiapo, anapaswa kutimiza ahadi yake. Anapaswa kushika yale yote aliyotamka kwa kinywa chake.
4Binti ambaye angali anaishi katika nyumba ya baba yake akiahidi mbele ya Yawe na kufanya kiapo,
5na baba yake akisikia ahadi hiyo naye hamupingi, yule binti atafungwa na kila kiapo na ahadi aliyofanya.
6Lakini kama baba yake akisikia juu ya kiapo hicho, akimupinga, basi kiapo chake au ahadi yake havitamufunga. Yawe atamusamehe kwa sababu baba yake amelipinga jambo hilo.
7Ikiwa binti ataolewa kisha kufanya kiapo au kuahidi bila kufikiri vizuri kwanza,
8halafu mume wake akisikia jambo hilo naye hamupingi, muke wake atafungwa na kila kiapo au ahadi aliyofanya.
9Lakini kama mume wake akisikia jambo hilo, akimupinga, basi huyo mume wake atavunja kiapo cha muke wake na maneno yale aliyosema bila kufikiri; naye Yawe atamusamehe.
10Lakini kiapo au ahadi yoyote mujane aliyoweka au mwanamuke aliyeachana na mume wake ambayo kwa njia yake amejifunga, inapaswa kumufunga.
11Mwanamuke aliyeolewa akifanya ahadi au kiapo akiwa katika nyumba ya mume wake,
12kisha mume wake akisikia jambo hilo naye hamupingi, wala kumwambia kitu, basi, viapo vyake vyote vitamufunga; vilevile na ahadi zake zote zitamufunga.
13Lakini kama mume wake atakaposikia habari zake, akizifunga na kuzivunja, basi, hata kama alitaka kutimiza kiapo au ahadi zake, hataombwa kuzitimiza. Mume wake atakuwa amezifunga na Yawe atamusamehe.
14Mume wake anaweza kuhakikisha au kufunga kiapo au ahadi yoyote inayomufunga.
15Lakini ikiwa mume wake hatasema neno lolote tangu siku atakaposikia habari za kiapo au ahadi ya muke wake, basi atakuwa ameihakikisha siku hiyo alipopata habari yake kwa sababu hakusema chochote.
16Lakini akiifunga na kuivunja muda fulani nyuma ya kusikia habari yake, basi yeye atabeba lazima ya kosa la muke wake.
17Haya ndiyo masharti ambayo Yawe alimwagiza Musa kati ya mume na muke wake, baba na binti yake, huyo binti akiwa bado kijana na anakaa katika nyumba ya baba yake.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.