1Nyuma ya Wafilistini kuliteka Sanduku la Mungu, walilibeba kutoka muji wa Ebeni-Ezeri mpaka katika muji wao wa Asidodi.
2Kisha, wakalipeleka Sanduku la Mungu kwenye hekalu la mungu wao Dagoni na kuliweka karibu naye.
3Kesho yake asubui, watu wa muji wa Asidodi walipoamuka waliona sanamu ya Dagoni imeanguka ikilalia uso chini mbele ya Sanduku la Mungu. Wakaisimamisha tena sanamu ya Dagoni na kuiweka tena pahali pake.
4Lakini, kesho yake asubui walipoamuka, waliona kwamba sanamu ya Dagoni imeanguka uso chini mbele ya Sanduku la Yawe, kichwa, miguu na mikono ya sanamu hiyo, vyote vilikuwa vimekatika, vikakuwa vimelala chini kwenye kizingiti cha mulango. Kiwiliwili cha sanamu ya Dagoni ndicho tu kilikuwa kimebakia.
5Ndiyo maana makuhani wa Dagoni na wote wanaoingia kumwabudu Dagoni kule Asidodi, wanapoingia kwenye hekalu la Dagoni hawakanyagi kizingiti cha hekalu la Dagoni mpaka leo.
6Yawe aliwaazibu vikali na kuwatisha watu wa Asidodi. Aliwaazibu, hata na wajirani zao, kwa kuwaletea ugonjwa wa majipu.
7Wakaaji wa Asidodi walipoyaona mambo yaliyowapata, wakasema: “Mungu wa Israeli anatuazibu vikali sisi pamoja na mungu wetu Dagoni. Sanduku la Agano la Yawe haliwezi kukaa kwetu.”
8Walituma wajumbe na kuwakusanya wakubwa wote wa Wafilistini na kuwauliza: “Tutafanya nini na Sanduku hili la Mungu wa Israeli?” Wakubwa wao wakajibu: “Sanduku hilo la Mungu wa Israeli mulipeleke Gati.” Basi, wakalipeleka kwenye muji wa Gati.
9Lakini kisha kulipeleka kule Gati, Yawe akauazibu muji huo, akitia hofu kubwa katika muji, na akawapiga wanaume wa muji huo, vijana kama vile wazee, kwa kuwaletea majipu.
10Hivyo, wakalipeleka Sanduku hilo la Mungu kwenye muji wa Ekuroni. Lakini Sanduku hilo la Mungu lilipofika kule, watu wa muji huo walipiga kelele: “Wametuletea Sanduku la Mungu wa Israeli kwa kutuua sisi na watu wetu.”
11Kisha wakatuma ujumbe na kukusanya wakubwa wa Wafilistini na kuwaambia: “Mulirudishe Sanduku la Mungu wa Israeli kwa nafasi yake, kusudi lisituue sisi pamoja na watu wetu.” Walifanya hivyo kwa sababu kulikuwa hofu kubwa katika muji muzima kwa sababu Mungu alikuwa anawaazibu vikali.
12Nao wale ambao hawakukufa walipatwa na majipu hata kilio cha muji kilifika mbinguni.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.