1Nyuma ya kifo cha Abimeleki, Tola mwana wa Puha mujukuu wa Dodo, wa kabila la Isakari, akatokea kuwakomboa Waisraeli. Tola aliishi Samiri katika inchi ya milima ya Efuraimu.
2Alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka makumi mbili na mitatu, kisha akakufa na kuzikwa kule Samiri.
Yairi3Nyuma ya Tola, kukatokea Yairi wa Gileadi, akakuwa mwamuzi wa Waisraeli kwa miaka makumi mbili na mbili.
4Yairi alikuwa na watoto wa kiume makumi tatu ambao walipanda juu ya punda makumi tatu na walikuwa na miji makumi tatu katika inchi ya Gileadi, ambayo mpaka leo inaitwa Miji ya Yairi.
5Yairi akakufa na kuzikwa kule Kamoni.
Yefuta6Waisraeli wakatenda tena uovu mbele ya Yawe, wakatumikia Mabali, Mastaroti, na miungu ya Aramu, ya Sidona, ya Moabu, ya Amoni na ya Wafilistini. Wakamwacha Yawe wala hawakumwabudu tena.
7Hasira ya Yawe ikawaka juu ya Waisraeli, naye akawatia katika mikono ya Wafilistini na Waamoni.
8Kwa miaka kumi na minane hao waliwatesa na kuwagandamiza Waisraeli walioishi kule Gileadi katika eneo la Waamori upande wa mashariki wa muto Yordani.
9Waamoni nao walivuka muto Yordani kupigana na makabila ya Yuda, Benjamina na Efuraimu. Nao Waisraeli wakapata taabu sana.
10Basi wakamulilia Yawe, wakisema: “Tumetenda zambi mbele yako, maana tumekuacha wewe Mungu wetu, tukatumikia Mabali.”
11Naye Yawe akawaambia: “Mimi sikuwakomboa kutoka kwa Wamisri, Waamoni, Waamori, na Wafilistini?
12Wasidoni, Waamaleki na Wamidiani waliwagandamiza nanyi mukanililia, nami nikawakomboa toka katika mikono yao.
13Hata hivyo ninyi mumeniacha, mukatumikia miungu mingine. Kwa hiyo sitawakomboa tena.
14Muende muililie hiyo miungu muliyoichagua. Muache hiyo iwakomboe katika taabu zenu!”
15Lakini Waisraeli wakamwambia Yawe: “Tumetenda zambi. Utufanye vile unavyopenda, lakini tunakuomba utuokoe leo.”
16Kisha wakaitupilia mbali miungu ya kigeni, wakamutumikia tena Yawe. Yawe hakuweza kuvumilia zaidi kuona taabu za Waisraeli.
17Waamoni wakajikusanya wakapiga kambi yao kule Gileadi. Waisraeli nao wakakusanyika na kupiga kambi yao kule Misipa.
18Waisraeli na viongozi wao wakaulizana: “Ni nani atakayeanza kupigana na Waamoni? Atakayefanya hivyo ndiye atakayekuwa kiongozi wa wakaaji wote wa Gileadi.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.