Mezali 7 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Mwana wangu, ushike maneno yangu,

uchunge amri zangu.

2Ufuate amri zangu nawe utaishi;

ulinde mafundisho yangu kama mboni ya jicho lako.

3Uyafunge kwenye vidole vyako;

uyaandike ndani ya moyo wako.

4Uambie Hekima: “Wewe ni dada yangu”,

na Akili: “Wewe ni rafiki yangu”.

5Vitakulinda mbali na mwanamuke mubaya,

vitakuepusha na maneno matamu ya mwanamuke mugeni.

6Siku moja katika dirisha ya nyumba yangu,

nilichungulia inje kupitia nyavu za dirisha,

7nikawaona vijana wengi wajinga,

na hasa mumoja aliyekuwa mupumbafu.

8Huyo alikuwa akitembea kwenye barabara ile,

karibu na pahali mwanamuke mumoja alipoishi.

Basi akashika njia inayokwenda kwa mwanamuke yule.

9Ilikuwa karibu wakati wa magaribi,

giza na usiku vilikuwa vimeanza kuingia.

10Kijana akakutana na yule mwanamuke;

alivaa kama kahaba, mwenye ukorofi.

11Alikuwa mwanamuke wa makelele na mwenye kiburi;

miguu yake haitulii ndani ya nyumba:

12mara katika barabara, mara katika soko,

pembeni ya njia hakosekani akivizia.

13Alimukumbatia kijana yule na kumubusu,

na kwa maneno matamu, akamwambia:

14“Ilinipasa kutoa sadaka zangu;

leo hii nimekamilisha naziri yangu.

15Ndio maana nimetoka kwa kukupokea,

nimekutafuta kwa hamu nikakupata.

16Nimetandika kitanda changu vizuri,

kwa blanketi za rangi za kitani kutoka Misri.

17Nimekinyuzia marasi, manemane, udi na mudalasini.

18Kuja! Tufanye mapenzi mpaka asubui;

kuja tujifurahishe kwa mapenzi.

19Mume wangu hayuko ndani ya nyumba,

amekwenda safari ya mbali.

20Amepeleka mufuko wa feza,

hatarudi mbele ya mwandamo wa mwezi.”

21Alimushawishi kwa maneno mengi ya kubembeleza;

kijana akashawishiwa kwa maneno yake matamu.

22Naye akamufuata yule mwanamuke moja kwa moja,

kama ngombe anayekwenda kuchinjwa,

kama mupambafu anayefungwa na kwenda kuazibiwa.

23Hakutambua kwamba maisha yake yako katika hatari,

mpaka alipojikuta amekuwa kama amechomwa mushale ndani ya moyo,

amekuwa kama ndege aliyerukia ndani ya wavu.

24Sasa wana wangu, munisikilize;

mutege sikio kwa maneno ya kinywa changu.

25Musikubali kuongozwa na mwanamuke kama yule,

wala musipitepite katika mapito yake.

26Maana amewaangusha wanaume wengi;

ni wengi sana wale aliowachinja.

27Nyumba yake ni njia ya kwenda kuzimu,

ni pahali pa kuteremukia katika mauti.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help