1Usijisifie kwa ajili ya kesho. Haujui siku ya leo itakuletea nini.
2Acha watu wengine wakusifu, kuliko kujisifu kwa mudomo wako wewe mwenyewe.
3Jiwe ni zito na muchanga vilevile, lakini uchokozi wa mupumbafu ni muzito zaidi.
4Kasirani ni kali na hasira inaangamiza; lakini ni nani anayeweza kupingana na wivu?
5Afazali mutu anayekuonya waziwazi, kuliko yule anayeficha upendo.
6Makaripio ya rafiki yanaonyesha uaminifu, lakini busu la adui ni udanganyifu.
7Aliyeshiba anakataa hata asali, lakini kwa mwenye njaa kila chakula kichungu ni kitamu.
8Mutu aliyepotea mbali na kwake ni kama ndege aliyepotea mbali na chicha yake.
9Mafuta na marasi vinafurahisha moyo, vilevile utamu wa urafiki kuliko kujitoshelea mwenyewe.
10Usisahau warafiki zako wala wa baba yako. Ukipatwa na magumu usikimbilie kwa ndugu yako. Afazali jirani ambaye iko karibu kuliko ndugu anayekuwa mbali.
11Ukuwe na hekima, mwana wangu, upate kunifurahisha moyo, nami sitakosa neno la kumujibu mutu yeyote anayenizarau.
12Mwenye akili anaona hatari na kujificha, lakini wajinga wanajitokeza mbele na kuumia.
13Mutu akiahidi mbele yako kubeba muzigo wa mutu mwingine, unyanganye nguo yake; utwae rehani kwake maana amebeba muzigo wa mutu mwingine.
14Anayemusalimia jirani yake kwa kelele asubui mapema, itahesabiwa kwamba amemutakia laana.
15Muke mugomvi ni kama matone ya mvua yasiyoisha siku ya mvua.
16Kumuzuia ni sawa na kuzuia upepo, au kukamata mafuta kwa mukono.
17Chuma kinanoa chuma, vilevile mutu anafundishwa na mwenzake.
18Anayetunza muti wa tini atakula matunda yake. Anayetumikia bwana wake ataheshimiwa.
19Kama uso unavyojiona wenyewe katika maji, ndivyo mutu anavyojijua mwenyewe ndani ya moyo.
20Kuzimu na shimo la kuangamia havishibi hata kidogo, vilevile macho ya watu hayashibi.
21Zahabu na feza vinapimwa kwa moto, na mutu anapimwa kutokana na sifa zake.
22Hata kama ukitwanga mupumbafu katika kinu, sawa na ngano, hautaweza kumutenganisha na upumbafu wake.
23Angalia vizuri hali ya makundi yako ya nyama; tunza vizuri nyama wako.
24Maana utajiri haudumu milele, wala taji haidumu kwa vizazi vyote.
25Nyuma ya kukata majani, wakati nyasi zinachipuka upya, kusanya majani toka kwenye milima.
26Kondoo watakupatia sufu kwa ajili ya nguo zako, mbuzi nao utawauzisha na kujinunulia mashamba;
27watakupa maziwa ya kukutoshelea na jamaa yako, na kwa ajili ya wajakazi wako.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.