1Yawe anasema hivi kwa Kiro, muchaguliwa wake:
Nilikuchagua kuwa mufalme kwa kunitumikia.
Ninaimarisha nguvu yako
kusudi uyashinde mataifa mbele yako,
na kuzivunja nguvu za wafalme.
Mimi ninafungua milango ya muji mbele yako,
na hakuna mulango utakaofungwa.
2Mimi nitakutangulia,
na kuisawanisha milima mbele yako.
Nitaivunjavunja milango ya shaba,
na kuvikatakata vifungio vyake vya chuma.
3Nitakupa akiba zilizofichwa
na mali inayokuwa pahali pa siri,
upate kutambua kwamba mimi ni Yawe,
Mungu wa Israeli, ninayekuita kwa jina lako.
4Kwa ajili ya mutumishi wangu Yakobo, muchaguliwa wangu Israeli,
nimekuita kwa jina lako;
nimekupa jina la heshima ingawa wewe haunijui.
5Mimi ni Yawe, wala hakuna mwingine;
hakuna Mungu mwingine lakini mimi.
Ninakuimarisha ingawa wewe haunijui,
6kusudi watu wote, toka mashariki mpaka magaribi,
wajue kwamba hakuna Mungu mwingine isipokuwa mimi tu.
Mimi ni Yawe na hakuna mwingine.
7Mimi ninafanya mwangaza na kuumba giza;
ninaleta uheri na kusababisha hasara.
Mimi Yawe ninatenda vitu hivi vyote.
8Enyi mbingu, munyeshe umande kutoka kule juu,
mawingu yatiririshe ushindi;
dunia ifuguke, ichipushe wokovu,
na kuotesha haki vilevile!
Mimi, Yawe nimefanya hayo.
Uwezo mukubwa wa Mungu9Ole kwake mutu anayebishana na Muumba wake:
chombo cha udongo kubishana na mufinyanzi wake!
Udongo unamwuliza anayeufinyanga:
Unatengeneza nini hapa?
au kumwambia: Kazi yako si kamili!
10Ole kwake mutu anayemwambia baba:
Umezaa nini?
au anayemwambia mama:
Umeleta nini katika dunia?
11Yawe, Mutakatifu wa Israeli,
Mungu, Muumba wa Israeli anasema hivi:
Munataka kuniuliza juu ya watoto wangu,
au kuniamuru juu ya kazi zangu mwenyewe?
12Ni mimi niliyeifanya dunia,
na kuumba mwanadamu anayeishi humo.
Mikono yangu ndiyo iliyozitandaza mbingu,
na kundi lote la nyota liko kwa amri yangu.
13Ni mimi niliyemwamuru Kiro akuje,
atimize mapenzi yangu.
Nitazifanikisha njia zake zote.
Ataujenga upya muji wangu Yerusalema,
na kuwapa uhuru watu wangu wanaokuwa katika uhamisho,
bila kutaka malipo wala zawadi.
–Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.
14Yawe anasema hivi:
Utajiri wa Misri na faida ya uchuuzi za Kushi,
pamoja na za watu wa Seba, wale watu warefu sana,
zitakuja kwako mwenyewe wewe taifa la Israeli,
zote zitakuwa mali yako.
Watu hao watakufuata wakifungwa minyororo;
watainama mbele yako na kukusihi wakisema:
Kwako kuna Mungu wa kweli,
wala hakuna Mungu mwingine lakini yeye.
15Kweli wewe ni Mungu mwenye kufichama,
Mungu wa Israeli, Mungu mwokozi.
16Watengenezaji wa sanamu watapata haya na kuzarauliwa,
wote pamoja watafezeheka.
17Lakini taifa la Israeli litaokolewa na Yawe,
litapata wokovu wa milele.
Halitapata haya wala kuzarauliwa milele.
18Hivi ndivyo anavyosema Yawe
aliyeumba mbingu,
ndiye Mungu
aliyeipa dunia umbo na kuifanya na kuiimarisha.
Hakuiumba kusudi ibaki ukiwa,
lakini aliipa umbo kusudi iikaliwe na viumbe vyake:
Mimi ni Yawe,
wala hakuna mwingine.
19Mimi sikusema kwa siri,
wala katika inchi yenye giza.
Mimi sikuwaambia wazao wa Yakobo
wanitafute pahali kusipokuwa kitu.
Mimi Yawe ninasema ukweli,
maneno yangu ni ya kuaminika.
20Enyi watu wa mataifa muliobaki,
mukusanyike pamoja mukuje!
Ninyi mumekosa akili:
ninyi munabeba sanamu za miti
na kumwomba mungu asiyeweza kuokoa watu.
21Mutangaze na kusema habari zenu.
Mufanye shauri pamoja!
Ni nani aliyetangaza zamani matukio ya sasa?
Ni nani aliyesema mambo haya zamani?
Haikukuwa mimi Yawe?
Hakuna Mungu mwingine isipokuwa mimi!
Mimi ni Mungu wa haki na mwokozi;
hakuna mwingine isipokuwa mimi.
22Munigeukie mimi mupate kuokolewa,
popote munapokuwa katika dunia.
Maana mimi ni Mungu, wala hakuna mwingine.
23Mimi nimeapa kwa nafsi yangu,
ninachosema ni ukweli,
neno langu halitarudi nyuma:
kila mwanadamu atanipigia magoti,
kila mutu atafanya kiapo.
24Watasema juu yangu:
Haki na nguvu viko kwa Yawe peke yake.
Wote waliomukasirikia Yawe
watakuja kwake na haya.
25Lakini wazao wa Israeli
watapata ushindi toka kwa Yawe na kufurahi.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.