1Barua hii inatoka kwangu mimi Simoni Petro, mutumishi na mutume wa Yesu Kristo. Ninawaandikia ninyi mulioshiriki pamoja nasi katika imani ile inayokuwa kubwa kwa njia ya haki ya Mungu wetu na Mwokozi Yesu Kristo.
2Ninawatakia neema na amani kwa uwingi kufuatana na vile munavyomujua Mungu na Yesu Bwana wetu.
Mwito wa kuchaguliwa na Mungu3Kwa uwezo wake, Mungu ametujalia mambo yote tunayohitaji katika maisha yetu kusudi tupate kushikamana na kumwabudu yule aliyetuita kushiriki utukufu wa wema wake mwenyewe.
4Kufuatana na hayo, ametupatia ahadi nzuri sana na kubwa mupate kuepuka uharibifu unaoletwa na tamaa mbaya za dunia na kushika hali yake ya kimungu.
5Na kwa sababu hii, mufanye bidii ya kuongeza wema juu ya imani yenu, elimu juu ya wema wenu,
6ukadirifu juu ya elimu yenu, uvumilivu juu ya ukadirifu, kushikamana na ibada juu ya uvumilivu,
7undugu juu ya kushikamana na ibada, na upendo juu ya undugu wenu.
8Kwa maana mukiwa na tabia hizi zote kwa uwingi, zitawawezesha kutumika na kuzaa matunda hata mupate kumujua Bwana wetu Yesu Kristo.
9Lakini mutu asiyekuwa na tabia hizo ni kipofu, hawezi kuona. Yeye amesahau kwamba amekwisha kutakaswa zambi zake za zamani.
10Kwa hiyo wandugu zangu, kufuatana na vile mulivyochaguliwa na kuitwa na Mungu, mufanye nguvu zaidi kwa kukamilika katika njia ile. Mukitenda mambo yale hamutaanguka hata kidogo.
11Maana kwa kufanya vile, mutaruhusiwa kabisa kuingia katika Ufalme wa milele wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo.
12Kwa sababu hii, nitaendelea kuwakumbusha mambo haya siku zote ingawa mumekwisha kuyafahamu na kukamilika katika ukweli muliopokea.
13Ninaona kwamba ni vema niwaamushe kwa njia ya kuwakumbusha mambo haya wakati wote wa maisha yangu.
14Kwa maana ninajua kwamba ninakaribia kuacha mwili huu unaokuwa wa kufa kama vile Bwana wetu Yesu Kristo alivyonionyesha waziwazi.
15Nitajikaza sana kuwapatia njia ya kuweza kukumbuka mambo haya siku zote kisha kufa kwangu.
Walioshuhudia utukufu wa Kristo16Basi, wakati tulipowajulisha uwezo na kurudia kwa Bwana wetu Yesu Kristo, sisi hatukutumia hadisi za uongo zilizotungwa kwa werevu. Lakini tulijionea na macho yetu sisi wenyewe uwezo wake.
17Maana alipokea heshima na utukufu toka kwa Mungu Baba, wakati sauti yenye utukufu mukubwa toka kwa Mungu ilipomufikia ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa, ninapendezwa naye sana!”
18Sisi wenyewe tuliisikia sauti ile toka mbinguni tulipokuwa pamoja naye juu ya mulima mutakatifu.
19Vilevile tunaamini ujumbe uliotangazwa na manabii. Ninyi munafanya vema mukishikamana nao. Ujumbe huo ni kama taa inayoangaza pahali pa giza, mpaka wakati wa mapambazuko na wakati nyota ya asubui itakapoangazia mioyo yenu.
20Mbele ya yote, mujue kwamba hakuna mutu anayeweza kufasiria yeye mwenyewe unabii unaokuwa katika Maandiko Matakatifu.
21Maana hakuna hata ujumbe wowote uliotetewa kwa mapenzi ya kimutu, lakini watu walipasha ujumbe wa Mungu wakiongozwa na Roho Mutakatifu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.