Isaya 31 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Misri haitaweza kusaidia

1Ole kwao wale wanaokwenda Misri kuomba musaada!

Wanategemea farasi,

wanategemea wingi wa magari ya vita

na nguvu za waaskari wao wapanda-farasi.

Lakini hawamutegemei Mutakatifu wa Israeli,

wala hawamwombi Yawe shauri!

2Mungu ni mwenye hekima na analeta maangamizi.

Habadilishi masemi yake;

lakini yuko tayari kuwaazibu watu waovu

vilevile na wasaidizi wa watenda mabaya.

3Wamisri ni wanadamu tu wala si miungu;

farasi wao nao ni nyama tu, si roho.

Yawe akiunyoosha mukono wake,

taifa linalotoa musaada litajikwaa,

na lile linalosaidiwa litaanguka;

yote mawili yataangamia pamoja.

Mungu ataulinda Yerusalema

4Yawe aliniambia hivi:

Simba mukali ananguruma

kwa kukinga nyama aliyemukamata;

hata kundi la wachungaji likiitwa kwa kumufukuza,

hatishiki kwa kelele zao,

wala hashituki kwa sauti zao.

Ni vile Yawe wa majeshi atakavyoshuka

kupigana juu ya mulima Sayuni na kilima chake.

5Kama vile ndege anavyonyoosha mabawa juu ya vitoto vyake,

ni vile Yawe atakavyolinda Yerusalema.

Ataulinda na kuukomboa,

ataukinga na kuuokoa.

6Enyi Waisraeli, mumurudilie yule muliyemwacha kabisa.

7Wakati utafika ambapo ninyi wote mutatupilia mbali sanamu zenu za feza na zahabu ambazo mumejitengenezea kwa mikono yenu inayowakosesha.

8Hapo Waasuria watauawa kwa upanga,

lakini si upanga wa watu;

wataangamizwa kwa upanga

ambao ni zaidi ya ule wa wanadamu.

Waasuria watakimbia

na vijana wao watatumikishwa kazi za kitumwa.

9Mufalme wao atatoroka kwa ajili ya hofu,

na wakubwa wao wataiacha bendera yao kwa ajili ya woga.

–Ni ujumbe wa Yawe ambaye moto wake uko katika Sayuni, ambaye furu lake liko katika Yerusalema.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help