1Ole kwao wale wanaokwenda Misri kuomba musaada!
Wanategemea farasi,
wanategemea wingi wa magari ya vita
na nguvu za waaskari wao wapanda-farasi.
Lakini hawamutegemei Mutakatifu wa Israeli,
wala hawamwombi Yawe shauri!
2Mungu ni mwenye hekima na analeta maangamizi.
Habadilishi masemi yake;
lakini yuko tayari kuwaazibu watu waovu
vilevile na wasaidizi wa watenda mabaya.
3Wamisri ni wanadamu tu wala si miungu;
farasi wao nao ni nyama tu, si roho.
Yawe akiunyoosha mukono wake,
taifa linalotoa musaada litajikwaa,
na lile linalosaidiwa litaanguka;
yote mawili yataangamia pamoja.
Mungu ataulinda Yerusalema4Yawe aliniambia hivi:
Simba mukali ananguruma
kwa kukinga nyama aliyemukamata;
hata kundi la wachungaji likiitwa kwa kumufukuza,
hatishiki kwa kelele zao,
wala hashituki kwa sauti zao.
Ni vile Yawe wa majeshi atakavyoshuka
kupigana juu ya mulima Sayuni na kilima chake.
5Kama vile ndege anavyonyoosha mabawa juu ya vitoto vyake,
ni vile Yawe atakavyolinda Yerusalema.
Ataulinda na kuukomboa,
ataukinga na kuuokoa.
6Enyi Waisraeli, mumurudilie yule muliyemwacha kabisa.
7Wakati utafika ambapo ninyi wote mutatupilia mbali sanamu zenu za feza na zahabu ambazo mumejitengenezea kwa mikono yenu inayowakosesha.
8Hapo Waasuria watauawa kwa upanga,
lakini si upanga wa watu;
wataangamizwa kwa upanga
ambao ni zaidi ya ule wa wanadamu.
Waasuria watakimbia
na vijana wao watatumikishwa kazi za kitumwa.
9Mufalme wao atatoroka kwa ajili ya hofu,
na wakubwa wao wataiacha bendera yao kwa ajili ya woga.
–Ni ujumbe wa Yawe ambaye moto wake uko katika Sayuni, ambaye furu lake liko katika Yerusalema.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.