1 Mambo ya Siku 24 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Kazi za makuhani

1Hayo ndiyo makundi ya wana wa Haruni. Haruni alikuwa na wana wane: Nadabu, Abihu, Eleazari na Itamari.

2Nadabu na Abihu walikufa mbele ya baba yao, wala hawakukuwa na watoto; kwa hiyo wandugu zao Eleazari na Itamari wakakuwa makuhani. Ang. Law 10.1-2

3Mufalme Daudi akawapanga wana wa Haruni katika makundi kufuatana na kazi zao. Alisaidiwa kufanya hivyo na Zadoki, wa uzao wa Eleazari, na Ahimeleki, wa uzao wa Itamari.

4Kwa vile ambavyo kulipatikana viongozi wanaume wengi zaidi kati ya wazao wa Itamari, wakawagawanya wana wa Eleazari chini ya viongozi kumi na sita, na wana wa Itamari chini ya viongozi wanane.

5Waligawanywa kwa kupiga kura maana kulikuwa wakubwa wa Pahali Patakatifu na viongozi wa Mungu kati ya ukoo zote mbili; ukoo wa Eleazari na ukoo wa Itamari.

6Naye Semaya mwana wa Nataneli, mwandishi, aliyekuwa Mulawi, akawaandika mbele ya mufalme Daudi, wakubwa wake, kuhani Zadoki, Ahimeleki mwana wa Abiatari na viongozi wa jamaa za makuhani na za Walawi; ukoo wa Eleazari ukatwaliwa kwa kupiga kura mbili na ukoo wa Itamari kwa kupiga kura moja.

7-18Kura ya kwanza ikamwangukia Yoyaribu,

ya pili Yedaya,

ya tatu Harimu,

ya ine Seorimu,

ya tano Malkia,

ya sita Miyamini,

ya saba Hakosi,

ya nane Abiya,

ya kenda Yesua,

ya kumi Sekania,

ya kumi na moja Eliasibu,

ya kumi na mbili Yakimu,

ya kumi na tatu Hupa,

ya kumi na ine Yesebeabu,

ya kumi na tano Bilga,

ya kumi na sita Imeri,

ya kumi na saba Heziri,

ya kumi na nane Hapisesi,

ya kumi na kenda Petahia,

ya makumi mbili Yehezekeli,

ya makumi mbili na moja Yakini,

ya makumi mbili na mbili Gamuli,

ya makumi mbili na tatu Delaya,

ya makumi mbili na ine Mazia.

19Hawa waliandikishwa kulingana na kazi zao kuingia katika nyumba ya Yawe kutumika kwa kadiri ya utaratibu waliowekewa na babu yao Haruni, kama vile alivyoamuriwa na Yawe, Mungu wa Israeli.

Majina ya Walawi

20-30Hawa ndio wazao wengine wa Lawi:

Mumoja wa wazao wa Aramu alikuwa: Subaeli.

Mumoja wa wazao wa Subaeli alikuwa: Yedeya.

Mumoja wa wazao wa Rehabia alikuwa: Isia kiongozi wa ukoo.

Mumoja wa wazao wa Isia alikuwa: Selemoti.

Mumoja wa wazao wa Selemoti alikuwa: Yahati.

Wana wa Hebroni walikuwa: Yeria, muzaliwa wa kwanza; Amaria, wa pili; Yahazieli, wa tatu; Yekameamu, wa ine.

Mwana wa Uzieli alikuwa: Mika.

Mumoja wa wazao wa Mika alikuwa: Samire.

Mumoja wa wazao wa Isia, ndugu ya Mika, alikuwa: Zekaria.

Wana wa Merari walikuwa: Mali, Musi, na Yazia.

Wana wa Merari toka kwa Yazia walikuwa: Soiamu, Zakuri na Ibiri.

Wana wa Mali walikuwa: Eleazari ambaye hakukuwa na mwana na Kisi ambaye mwana wake alikuwa Yerameli.

Wana wa Musi walikuwa: Mali, Ederi na Yeremoti.

Wao ni wazao wa Lawi kulingana na ukoo zao.

31Vilevile hao wote walipiga kura kufuatana na ukoo wa kila mukubwa na mudogo wake, kama vile wazao wa Haruni walivyofanya. Walipiga kura mbele ya mufalme Daudi, Zadoki, Ahimeleki na viongozi wa jamaa za makuhani na za Walawi.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help