1Siku moja wakubwa wamoja wa Waisraeli walinitembelea kwa kutaka shauri.
2Basi neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
3Wewe mwanadamu, watu hawa wamekubali mioyo yao itawaliwe na sanamu za miungu; miungu hiyo inawasukuma kutenda zambi. Nitakubali kuulizwa shauri nao?
4Basi, sema nao uwaambie kwamba Bwana wao Yawe anasema: Mutu yeyote kati ya Waisraeli anayekubali sanamu za miungu zimutawale ndani ya moyo, na kuiruhusu miungu hiyo kumusukuma kutenda zambi, kisha akuje kumwomba nabii shauri, atapata jibu toka kwangu ambalo litafalia hata kwa sanamu zake nyingi za miungu.
5Mimi Yawe nitaigusa mioyo ya Waisraeli kusudi wanirudilie, maana wamejitenga mbali nami kwa kuabudu sanamu zao za miungu.
6Basi, uwaambie Waisraeli kwamba:
Bwana wetu Yawe anasema hivi: Munirudilie, na kuacha kuziabudu sanamu zenu za miungu. Muache kufanya machukizo.
7Wakati wowote mutu mumoja kati ya Waisraeli au mugeni yeyote anayekaa katika inchi ya Waisraeli, anapojitenga nami na kuanza kuziabudu sanamu za miungu kwa bidii na zambi hiyo ikiwa kizuizi kati yangu naye, halafu akimwendea nabii kusudi ajue mapenzi yangu, basi, mimi Yawe mwenyewe, nitamujibu mutu yule.
8Nitapingana naye. Nitamufanya kuwa kitambulisho na mufano; nitamwondoa kabisa kutoka taifa langu. Halafu mutatambua kwamba mimi ni Yawe.
9Na ikiwa nabii yule akidanganyika na kusema kitu, basi mimi Yawe nimemupotosha. Nami nitanyoosha mukono wangu kwa kumwondoa nabii yule kutoka kwa watu wangu Waisraeli.
10Nitamwazibu yule nabii pamoja na yule mutu aliyekuja kumwuliza mapenzi yangu; wote watapata azabu ileile.
11Kwa hiyo Waisraeli hawataniacha tena na kujichafua wenyewe kwa kutenda zambi; kusudi wakuwe watu wangu nami nikuwe Mungu wao.
–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
Noa, Daneli na Yobu12Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:
13Wewe mwanadamu! Taifa fulani likitenda zambi kwa kukosa uaminifu kwangu, mimi nitanyoosha mukono wangu kwa kuliazibu. Nitaiharibu akiba yake ya chakula na kuliletea njaa. Nitawaua watu na nyama wake.
14Hata kama Noa, Danieli na Yobu wangalikuwa ndani ya inchi ile, wangeyaokoa tu maisha yao wenyewe kwa ajili ya haki yao. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–
15Tena nitatuma nyama wa pori katika inchi hiyo na kuwanyanganya watoto wao na kuifanya inchi hiyo kuwa ukiwa, hata hakuna mutu yeyote atakayeweza kupita katika inchi ile kwa sababu ya nyama wakali.
16Hata kama hao watu watatu wangalikuwa ndani ya inchi ile, kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– hawangeweza kuwaokoa hata wana au wabinti zao. Wao wenyewe tu wangeokolewa, lakini inchi ile ingekuwa ukiwa.
17Tena nitaleta vita juu ya inchi ile na kuamuru waiangamize na kuua watu na nyama wanaokuwa ndani yake.
18Hata kama hao watu watatu wangalikuwa ndani ya inchi ile, kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– hawangeweza kuwaokoa hata wana au wabinti zao. Wao wenyewe tu wangeokolewa.
19Tena nitaleta ugonjwa mukali katika inchi ile na kwa kasirani yangu nitawaua watu na nyama.
20Na hata kama Noa, Daneli na Yobu wangelikuwa ndani ya inchi ile, kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– hawangeweza kuwaokoa hata mwana au binti. Wangeyaokoa tu maisha yao wenyewe kwa ajili ya haki yao.
21Lakini Bwana wetu Yawe anasema: Tena nitauazibu Yerusalema kwa mapigo yangu mane ya hukumu kali: vita, njaa, nyama wakali na ugonjwa mukali, nipate kuangamiza watu na nyama ndani yake! Ang. Ufu 6.8
22Hata hivyo, kutabaki wazima watu watakaoponyoka na kuwaleta wana na wabinti zao kwako, wewe Ezekieli. Utaona jinsi wanavyokuwa waovu sana; nawe utakubali kwamba azabu yangu juu ya Yerusalema ni ya haki.
23Mienendo na matendo yao vitakuhakikishia kwamba hasara niliyouletea muji huo sikuileta bila sababu. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.