1Mara tu Atalia mama ya mufalme Ahazia alipoona kwamba mwana wake ameuawa, alitoka, akaangamiza watu wote wa jamaa ya kifalme.
2Lakini Yoseba binti ya mufalme Yoramu, dada ya Ahazia, alimutwaa kwa siri Yoasi mwana wa Ahazia, kutoka kati ya wana wa mufalme waliokuwa karibu kuuawa. Alimuficha yeye pamoja na mulezi wake katika chumba cha kulala. Hivyo walimuficha kusudi Atalia asimwone na kumwua.
3Yoasi alikaa naye kwa muda wa miaka sita akiwa amefichwa ndani ya nyumba ya Yawe, wakati Atalia alipokuwa akitawala katika inchi.
4Lakini katika mwaka wa saba Yehoyada alituma ujumbe na kuwakusanya wakubwa wa waaskari na walinzi. Akaamuru wamufikie katika nyumba ya Yawe, naye akafanya nao mapatano na kuwaapisha humo katika nyumba ya Yawe. Halafu akawaonyesha Yoasi mwana wa mufalme Ahazia.
5Kisha akatoa amri: “Mutafanya hivi: mutakapokuja kushika zamu siku ya Sabato, sehemu moja ya tatu italinda nyumba ya kifalme,
6sehemu ingine moja ya tatu itakuwa kwenye mulango wa Suri na sehemu ingine itakuwa kwenye mulango nyuma ya walinzi. Hivi ndivyo mutakavyolinda nyumba ya kifalme kusudi isivunjwe.
7Yale makundi mawili ambayo yanamaliza zamu yao siku ya Sabato yatashika zamu katika nyumba ya Yawe kwa kumulinda mufalme.
8Mutamuzunguka mufalme, kila mutu na silaha yake katika mukono na mutu yeyote atakayesubutu kuwakaribia mumwue. Mukae na mufalme, ikiwa anatoka au anaikaa.”
9Wakubwa walitii amri zote kuhani Yehoyada alizotoa. Kila mukubwa akakamata watu wake wote, wale waliokuwa wamemaliza zamu na wale waliokuwa wanaingia kushika zamu siku ya Sabato, basi wakamwendea kuhani Yehoyada.
10Kisha kuhani akawapa wakubwa mikuki na ngao zilizokuwa mali ya mufalme Daudi, na ambazo zilikuwa zimewekwa katika nyumba ya Yawe,
11nao walinzi walisimama kuanzia upande wa kusini wa nyumba mpaka upande wa kaskazini wa nyumba na kuzunguka mazabahu na nyumba kwa kumuzunguka mufalme; kila mutu akiwa ameshika mukuki wake katika mukono.
12Halafu Yehoyada akamutoa inje mwana wa mufalme, akamuvalisha taji juu ya kichwa, na kumupa maandiko ya sheria. Wakamuweka kuwa mufalme na kumupakaa mafuta. Wakapiga mikono na kusema: “Mufalme aishi milele!”
13Naye Atalia aliposikia sauti za walinzi pamoja na za watu wengine, aliwaendea wale watu waliokuwa katika nyumba ya Yawe.
14Alipochungulia akamwona mufalme mupya akisimama karibu na nguzo kwenye kiingilio cha hekalu kama ilivyokuwa desturi nao wakubwa wa waaskari na wapiga baragumu wakiwa pembeni ya mufalme, na wakaaji wote wakishangilia na kupiga baragumu. Basi, akapasua nguo zake na kusema kwa sauti kubwa: “Uasi! Uasi!”
15Kisha kuhani Yehoyada akaamuru wakubwa wa waaskari akisema: “Mumwondoshe inje katikati ya waaskari, na muue mutu yeyote atakayemufuata.” Kwa sababu kuhani alisema: “Asiuawe katika nyumba ya Yawe.”
16Basi, wakamukamata, wakamupeleka na kumupitisha kwenye Mulango wa Farasi kuelekea nyumba ya kifalme, naye akauawa kule.
Mabadiliko ya Yehoyada(2 Sik 23.16-21)17Kisha Yehoyada akafanya agano kati ya Yawe na mufalme na watu kwamba watakuwa watu wa Yawe. Vilevile alifanya agano kati ya mufalme na watu.
18Halafu wakaaji wakaenda kwenye nyumba ya Bali na kuibomoa, wakavunja mazabahu pamoja na sanamu zake, hata wakamwua Matani, kuhani wa Bali mbele ya mazabahu. Kuhani Yehoyada akaweka walinzi kwa kulinda nyumba ya Yawe.
19Aliwakamata wakubwa wa waaskari, waaskari walinzi na watu wote, nao wakamusindikiza mufalme kutoka nyumba ya Yawe, wakapitia katika mulango wa walinzi mpaka kwenye nyumba ya kifalme. Naye mufalme akakiikalia kiti cha kifalme.
20Kwa hiyo, watu wote walipata furaha na muji wote ulikuwa mutulivu, nyuma ya Atalia kuuawa kwa upanga katika nyumba ya kifalme.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.