1Musa akawaita pamoja Waisraeli wote akawaambia: “Muliona ninyi wenyewe jinsi Yawe alivyomutendea mufalme wa Misri, wakubwa, watumishi wake na inchi yake yote.
2Muliona majaribu makubwa, vitambulisho na maajabu aliyotenda.
3Lakini mpaka leo Yawe hajawapa ninyi akili ya kuelewa, macho ya kuona, wala masikio ya kusikia!
4“Kwa muda wa miaka makumi ine, mimi niliwaongoza katika jangwa, nguo zenu mulizovaa hazikuchakaa wala viatu vyenu havikuchakaa kwenye miguu yenu.
5Hamukukula mukate wala kunywa divai au kileo chochote. Na hivyo mutapata kujua kwamba Yawe ni Mungu wenu.
6“Na mulipofika pahali hapa, mufalme Sihoni wa Hesiboni na mufalme Ogi wa Basani walikuja kupigana nasi; lakini tukawashinda,
7tukakamata inchi yao, tukayagawanyia makabila ya Rubeni na Gadi na nusu kabila la Manase ikuwe mali yao.
8Kwa hiyo mukuwe waangalifu kushika maneno yote ya agano hili kusudi mupate kufanikiwa katika kazi zenu zote.
9“Leo, mumesimama mbele ya Yawe, Mungu wenu, ninyi wote viongozi wa makabila, wazee wenu, wakubwa wenu,
10watoto wenu na wake zenu, wageni wanaoishi kati yenu ambao wanakata kuni na kuwatekea maji.
11Muko hapa leo kwa kufanya agano pamoja na Yawe, Mungu wenu na kulihakikisha kwa kiapo.
12Kwa hiyo leo mutakuwa watu wake naye atakuwa Mungu wenu, kama vile alivyowaapia ninyi na babu zenu Abrahamu, Isaka na Yakobo.
13Wala sifanyi agano hili leo kwa ajili yenu tu na kutamka laana zake; sifanyi kwa ajili ya wale tu wanaokuwa pamoja nasi leo mbele ya Yawe, Mungu wetu
14lakini vilevile kwa ajili ya wale ambao hawapo pamoja nasi leo.
15“Munajua jinsi tulivyoishi katika inchi ya Misri na jinsi tulivyosafiri katika inchi za mataifa mengine.
16Muliona sanamu zao za kuchukiza, miungu ya miti na mawe, ya feza na zahabu.
17Mufanye angalisho kwamba hakuna mwanaume, mwanamuke, jamaa au kabila lolote linalosimama hapa leo litakalomwacha Yawe, Mungu wetu, kwenda kutumikia miungu ya mataifa mengine. Jambo hili litakuwa kama muzizi utakaoota na kuzaa matunda machungu yenye sumu.
18Kisha kusikia maneno ya agano hili ambayo mumeapishwa, na mutu akijiamini mwenyewe ndani ya moyo wake na kusema atakuwa salama naye akifuata ugumu wake, hiyo italeta maangamizi.
19Yawe hatasamehe mutu huyo, nayo hasira ya Yawe na wivu wake vitamuwakia mutu huyo. Laana zote zilizoandikwa katika kitabu hiki zitamupata, naye Yawe atafuta kabisa jina la mutu huyo kutoka katika dunia.
20Yawe atamutenga kutoka kati ya makabila yote ya Israeli apatwe na hasara kufuatana na laana zote za agano zilizoandikwa katika kitabu hiki.
21Katika vizazi vinavyokuja, wazao wenu na wageni kutoka inchi ya mbali wataona jinsi Yawe alivyoletea inchi hii hasara na mateso.
22Wataona kwamba imejaa kiberiti na chumvi, imechomwa na kuwa tupu, haikupandwa mbegu na haioti chochote. Ni kama vile ilivyokuwa wakati Yawe alipoangamiza Sodoma na Gomora, Adima na Seboimu, kwa hasira yake kali.
23Hata mataifa yote yatasema: ‘Kwa nini Yawe ameitendea hivyo inchi hii? Hasira hii kubwa ina maana gani?’
24Na jibu hili litatolewa: ‘Ni kwa sababu walivunja agano la Yawe, Mungu wa wazee wao ambalo alifanya nao alipowatoa katika inchi ya Misri.
25Wakaenda kutumikia na kuabudu miungu mingine, ambayo hawakuijua mbele, wala Yawe hakukuwa amewapa.
26Kwa hiyo hasira ya Yawe ikawaka juu ya inchi hii, na kuiletea laana zote zilizoandikwa katika kitabu hiki.
27Naye Yawe, akawaongoza kutoka katika inchi yao kwa hasira na kasirani kubwa, akawatupa katika inchi nyingine kama vile inavyokuwa leo’.
28“Mambo ya siri ni ya Yawe, Mungu wetu, lakini yale ambayo ameyafunua ni yetu na wazao wetu milele, kusudi tushike maneno yote ya sheria hii.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.