1Kisha watu wote wa Yuda wakamukamata Uzia mwana wa Amazia akiwa mwenye umri wa miaka kumi na sita, wakamufanya kuwa mufalme pahali pa Amazia baba yake.
2Halafu nyuma ya kifo cha baba yake akajenga upya muji wa Eloti na kuurudisha kwa inchi ya Yuda.
3Uzia alianza kutawala akiwa na umri wa miaka kumi na sita; akatawala kwa muda wa miaka makumi tano na miwili kule Yerusalema. Mama yake aliitwa Yekolia wa Yerusalema.
4Alitenda kwa usawa mbele ya Yawe, kama vile baba yake alivyotenda.
5Akamutumikia Yawe kwa uaminifu wakati wa kuishi kwa Zakaria, aliyemufundisha kumutii Mungu. Kwa jinsi alivyomutafuta Mungu, Mungu alimufanikisha.
6Uzia akaondoka kwa kupigana vita na Wafilistini, akabomoa kuta za miji ya Gati, Yabune na Asidodi. Akajenga miji katika eneo la Asidodi na fasi ingine katika inchi ya Filistia.
7Mungu akamusaidia kuwashinda Wafilistini, Waarabu waliokaa Guribali na Wameuni.
8Waamoni walimulipa kodi, na sifa zake zikaenea mpaka Misri, kwa sababu alipata nguvu.
9Tena Uzia akajenga minara ya kukinga muji kwenye milango tatu ya Yerusalema na kuiimarisha.
10Hata katika jangwa vilevile alijenga minara, akachimba visima vingi, maana alikuwa na makundi mengi ya nyama kwenye sehemu za miinuko na mabonde. Alikuwa na walimaji na watunza mizabibu kwenye milima, na katika inchi yenye mboleo maana alipenda mulimo.
11Zaidi ya hayo, Uzia alikuwa na jeshi lililokuwa tayari kwa vita. Lilikuwa limegawanywa katika vikundi mbalimbali, na jumla ya hesabu yao iliwekwa na katibu Yeieli, na Masea, mukubwa, nao wote walikuwa chini ya uongozi wa Hanania, mumoja wa majemadari wa mufalme.
12Kwa jumla, viongozi wote wa majeshi walikuwa elfu mbili na mia sita.
13Chini yao, kulikuwa jeshi la waaskari elfu mia tatu na saba na mia tano, wenye uwezo mukubwa wa kupigana na waadui wa mufalme.
14Uzia aliwapa waaskari wale ngao, mikuki, kofia za chuma, nguo za chuma, pinde na mawe kwa ajili ya kupiga mujeledi.
15Kule Yerusalema wafundi wake wakamutengenezea mitambo ya kurushia mishale na mawe makubwamakubwa. Sifa zake zikaenea kila pahali, nguvu zake zikaongezeka zaidi kwa sababu ya usaidizi mwingi alioupata kutoka kwa Mungu.
Uzia anaazibiwa kwa ajili ya majivuno yake16Lakini wakati mufalme Uzia alipokuwa na nguvu, moyo wake akajaa kiburi ambacho kilisababisha maangamizi yake. Akamwasi Yawe wake kwa kuingia ndani ya hekalu akikusudia kufukiza ubani juu ya mazabahu.
17Lakini kuhani Azaria, pamoja na makuhani wengine mashujaa makumi nane, wakamufuata mufalme
18na kumuzuia. Wakamwambia: “Si kazi yako hata kidogo Uzia, kumufukizia Yawe ubani. Ni makuhani tu wa uzao wa Haruni ambao wametakaswa kwa kufukiza ubani. Ondoka pahali hapa patakatifu. Umemukosea Yawe na hautapata heshima yoyote kutoka kwake.”
19Wakati ule, Uzia alikuwa amesimama ndani ya hekalu karibu na mazabahu, akishika chetezo cha kufukizia ubani katika mukono. Akawakasirikia makuhani; na mara tu alipofanya hivyo, akashikwa na ukoma katika paji la uso wake mbele ya makuhani hao.
20Azaria, Kuhani Mukubwa, na wale makuhani wengine, wakamwangalia, kisha wakaharakisha kumutoa inje; hata yeye mwenyewe akafanya haraka kutoka, kwa maana Yawe alikuwa amemwazibu.
21Basi mufalme Uzia akakuwa na ukoma mpaka siku ya kufa kwake. Alikaa katika nyumba yake ya pekee maana hakukubaliwa tena kuingia katika nyumba ya Yawe. Na Yotamu mutoto wake, akatunza jamaa yake akitawala wakaaji wa inchi.
22Matendo mengine yote ya mufalme Uzia kutoka mwanzo mpaka mwisho, yaliandikwa na nabii Isaya mwana wa Amozi.
23Uzia akakufa na kuzikwa katika eneo la kuzikia wafalme, kwa sababu walisema: “Yeye ana ukoma”. Naye Yotamu mwana wake, akatawala pahali pake.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.