Yeremia 5 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Zambi ya Yerusalema

1Mukimbie huko na huko katika Yerusalema,

mupeleleze na kujionea wenyewe,

muchunguze katika masoko yake.

Mukiona hata mutu mumoja anayefuata sheria,

mutu anayetafuta ukweli,

basi Yawe atausamehe Yerusalema.

2Ingawa watu wake wanaapa kwa nafsi ya Yawe,

viapo vyao ni vya uongo.

3Ee Yawe, wewe unatafuta uaminifu siku zote.

Umewatwanga, lakini hawakuona uchungu;

umewateketeza, lakini walikataa maonyo.

Wamevifanya vichwa vyao kuwa vigumu kuliko jiwe;

wamekataa kabisa kurudi kwako.

4Kwa hiyo niliwaza hivi:

Watu hawa ni zaifu, hawana akili;

hawajui mapenzi ya Yawe,

hawajui Sheria ya Mungu wao.

5Nitawaendea wakubwa niongee nao;

bila shaka, wao wanajua mapenzi ya Yawe;

wanajua sheria ya Mungu wao.

Lakini wote ni sawa.

Wamevunja nira yao,

wamekata minyororo yao.

6Kwa hiyo simba kutoka pori atawaua;

imbwa wa pori kutoka jangwa atawararua.

Chui anaivizia miji yao.

Kila mutu anayetoka humo atararuliwa vipandevipande,

kwa sababu zambi zao ni nyingi,

maasi yao ni makubwa.

7Yawe anauliza:

Namna gani nitaweza kukusamehe, ee Yerusalema?

Watu wako wameniasi;

wameapa kwa majina ya miungu ya uongo.

Nilipowashibisha kwa chakula,

wao walifanya uzinzi,

wakakusanyika kwa uwingi katika nyumba za makahaba.

8Walikuwa kama farasi dume wanono wenye tamaa,

kila mumoja anamutamani muke wa jirani yake.

9Basi, nisiwaazibu kwa ajili ya mambo haya yote?

–Ni ujumbe wa Yawe.–

Nisilipize kisasi juu ya taifa kama hili?

10Mupande, mupite katika mashamba yake ya mizabibu,

muharibu kila kitu lakini musivimalize kabisa.

Mukate matawi yake,

kwa maana hayo si yangu mimi Yawe.

11Kweli, watu wa Israeli na watu wa Yuda,

wamekosa kabisa uaminifu kwangu.

–Ni ujumbe wa Yawe.–

Matokeo ya kuachiliwa na Mungu

12Watu hao wamesema uongo juu ya Yawe.

Wamesema: Hatafanya kitu;

hatutapatwa na hasara yoyote;

hatutafikiwa na vita wala njaa.

13Manabii si kitu, ni upepo tu.

Maneno wanayoyasema hayatoki kwa Mungu.

Iwatokee kama vile wanavyosema!

14Yawe wa majeshi anasema hivi:

Kwa sababu wao wamesema jambo hilo,

sasa nitayafanya maneno niliyokupa wewe Yeremia kuwa moto.

Nao watu hawa watakuwa kuni,

na moto huo utawateketeza.

15Na kwa ngambo yenu ninyi watu wa Israeli,

ninaleta taifa moja kutoka mbali kuwashambulia.

–Ni ujumbe wa Yawe.–

Hili taifa haliwezi kushindwa,

ni taifa la zamani,

ni taifa ambalo hamufahamu luga yake.

Hamuwezi kuelewa hata neno wanalolisema.

16Mishale yao inaua watu kwa uwingi,

wote ni mashujaa wa vita.

17Watakula mazao yenu na chakula chenu;

watawaua wana na wabinti zenu.

Watachinja makundi yenu ya kondoo na ngombe;

wataiharibu mizabibu yenu na miti yenu ya matunda ya tini.

Miji yenu yenye kuzungukwa na kuta munayoitegemea,

wataiharibu kwa silaha zao.

18Lakini hata katika siku hizo

mimi, sitawaangamiza ninyi na kuwamaliza kabisa.

–Ni ujumbe wa Yawe.

19Na watu wenu watakapouliza: Kwa nini Yawe, Mungu wetu, ametutendea mambo hayo yote? Wewe Yeremia utawajibu hivi: Ninyi mulimwacha Yawe, mukaitumikia miungu ya kigeni katika inchi yenu. Basi ndivyo mutakavyowatumikia watu wengine katika inchi isiyokuwa yenu.

Mungu anawaonya watu wake

20Muwatangazie wazao wa Yakobo;

muwaambie hao watu wa Yuda hivi:

21Musikilize, enyi wajinga na wapumbafu:

ninyi munaokuwa na macho, lakini hamwoni,

munaokuwa na masikio, lakini hamusikii.

22Mbona hamuniogopi?

–Ni ujumbe wa Yawe.–

Kwa nini hamutetemeki mbele yangu?

Mimi niliwekea bahari muchanga kuwa mupaka wake;

ni kizuizo cha milele ambacho bahari haiwezi kuvuka.

Ingawa mawimbi yanaupiga, hayawezi kuupita;

ingawa yanavuma, hayawezi kuuruka.

23Lakini watu hawa wana moyo mugumu na wa uasi;

wamegeuka na kuniacha.

24Wala hawasemi wenyewe hivi:

Inatupasa kumwogopa Yawe, Mungu wetu,

anayetujalia mvua kwa wakati wake,

anayetupatia mvua za kwanza na mvua za mwisho;

na kutupatia nyakati nzuri za mavuno.

25Makosa yenu yamewazuia musipate baraka hizo,

zambi zenu zimewafungia kupata mema yale.

26Hakika, kati ya watu wangu kuna waovu,

watu ambao wananyanganya mali za wengine.

Wako kama wawindaji wa ndege:

wanatega mitego yao na kuwanasa watu.

27Kama vile kikapu kinachojaa ndege walionaswa,

ndivyo nyumba zao zinavyojaa mali za udanganyifu.

Ndiyo maana wamekuwa watu wakubwa na watajiri,

28wamenenepa na kungaa vizuri.

Maovu yao hayana mwisho,

hawahukumu yatima kwa kufuatana na sheria kusudi wapate kufanikiwa,

wala hawatetei haki za watu wakosefu.

29Mimi sitawaazibu kwa ajili ya mambo haya?

Nitaachilia taifa hili bila kulilipiza kisasi?

–Ni ujumbe wa Yawe.

30Jambo la ajabu na la kuchukiza

limetendeka katika inchi hii:

31manabii wanatabiri mambo ya uongo,

nao makuhani wanatafuta faida yao wenyewe;

nao watu wangu wanaona jambo hilo kuwa sawa.

Lakini mwisho wake utakapofika mutafanya nini?

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help