Ezekieli 41 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Kisha, yule mutu akanipeleka kwenye baraza la ndani, Pahali Patakatifu. Akaipima nafasi iliyoelekea humo ndani, nayo ilikuwa na urefu wa metre tatu,

2na upana wa metre tano. Nafasi hiyo ilikuwa na kuta kila upande zenye unene wa metre mbili na nusu. Akapima baraza lenyewe, nalo lilikuwa na urefu wa metre makumi mbili na upana metre kumi.

3Kisha akaenda kwenye chumba cha ndani kabisa. Akaipima nafasi iliyoelekea huko, nayo ilikuwa na kimo cha metre moja na upana metre tatu na nusu. Nafasi hiyo ilikuwa na kuta kila upande zenye unene wa metre tatu na nusu.

4Akakipima chumba chenyewe, nacho kilikuwa cha muraba pande zake zikiwa na upana wa metre kumi. Chumba hiki kilikuwa mbele ya baraza la katikati. Kisha, akaniambia: Hapa ndipo Pahali Patakatifu Sana.

Vyumba vilivyojengwa pembeni ya hekalu

5Yule mutu aliupima unene wa ukuta wa nyumba ya Yawe, nao ulikuwa metre tatu. Kulikuwa mufululizo wa vyumba vidogovidogo vilivyozunguka nyumba ya Yawe, vyenye upana wa metre mbili.

6Vyumba hivi vilikuwa katika majengo ya gorofi tatu, na kila gorofi ilikuwa na vyumba makumi tatu. Ukuta wa inje wa hekalu kila kwenye gorofi ulikuwa mwembamba kuliko ule wa gorofi ya chini, kusudi vile vyumba vikuwe imara bila kuutegemea ukuta wa hekalu.

7Kwa upande, zile kuta za hekalu zikitazamwa kutokea inje, zilionekana kuwa na unene uleule toka chini mpaka juu. Kuelekea ukuta wa inje wa nyumba ya Yawe, inje ya vyumba, kulikuwa ngazi mbili, ambazo zilifanya ikuwe vyepesi kwenda juu kutokea gorofi ya chini mpaka ile ya juu.

8Kisha, nikaona kwamba hekalu lilikuwa likizungukwa na sakafu iliyonyanyuliwa, nayo ilikuwa ndio musingi wa zile gorofi tatu mbele ya hekalu, kimo cha musingi wa gorofi hizo ulikuwa sawa na ule ufito wa kupimia, metre tatu.

9Unene wa ukuta wa inje wa vyumba vya ndani ulikuwa metre mbili na nusu. Nafasi wazi kati ya vyumba vya pembeni mbele ya hekalu

10na vyumba vya walinzi vilikuwa na upana wa metre kumi, kuzunguka hekalu.

11Kulikuwa milango kwenye vyumba vya pembeni kutokea kwenye kiwanja, mumoja upande wa kaskazini na mwingine upande wa kusini. Na musingi uliounganishwa na kiwanja ulikuwa na upana wa metre mbili na nusu.

Jengo la upande wa magaribi

12Kwa mwisho kabisa wa kiwanja, upande wa magaribi kulikuwa jengo lenye urefu wa metre makumi ine na tano na upana wa metre makumi tatu na tano. Kuta zake zilikuwa na unene wa metre mbili na nusu.

Jumla ya vipimo vya jengo la hekalu

13Yule mutu akapima upande wa inje wa hekalu nao ulikuwa na urefu wa metre makumi tano. Tokea nyuma ya nyumba ya Yawe kupitia ile nafasi ya kupitia, mpaka mwisho wake, upande wa magaribi, umbali wake ulikuwa vilevile metre makumi tano.

14Urefu mbele ya hekalu tangu upande huu mpaka upande huu ukichanganya na ile nafasi wazi, ulikuwa vilevile metre makumi tano.

15Yule mutu akapima urefu wa jengo mpaka magaribi pamoja na mabaraza yake pande zake zote, nalo lilikuwa na urefu wa metre makumi tano.

Maelezo juu ya jengo la hekalu

Chumba cha kuingilia katika hekalu, Pahali Patakatifu, na Pahali Patakatifu Sana,

16vyote vilipambwa kwa mbao tangu kwenye sakafu mpaka kwenye madirisha. Madirisha haya yangeweza kufunikwa.

17Mpaka kwenye nafasi juu ya mulango hata kwenye chumba cha ndani na inje yake, vilevile juu ya kuta ndani ya chumba cha ndani na kwenye baraza kulikuwa michoro iliyofanana na

18miti ya gazi na picha za makerubi. Kisha kila muti wa ngazi kulichorwa picha ya kerubi kukizunguka chumba chote. Kila kerubi alikuwa na nyuso mbili:

19uso wa mwanadamu ulioelekea kwenye muti wa ngazi upande mumoja na uso wa simba ulioelekea kwenye muti wa ngazi upande mwingine. Hivi ndivyo ilivyokuwa kwenye nyumba nzima,

20tangu sakafu mpaka juu ya milango kulichorwa makerubi na miti ya ngazi.

21Miimo ya Pahali Patakatifu ilikuwa ya muraba.

Mazabahu ya mbao

Mbele ya mulango wa kuingilia Pahali Patakatifu Sana kulikuwa kitu kilichoonekana kama

22mazabahu ya mbao. Urefu wake kwenda juu ulikuwa metre moja na nusu na upana wa metre moja. Pembe zake, tako lake, na pande zake zote zilikuwa zimetengenezwa kwa mbao. Yule mutu akaniambia hivi: Hii ndiyo meza inayokaa mbele ya Yawe.

Milango

23Kulikuwa mulango wa kuingia kwenye baraza la hekalu na mulango wa kuingia kwenye Pahali Patakatifu Sana.

24Milango hiyo ilikuwa na sehemu mbilimbili, kwa hiyo kila mulango uliweza kufunguka katikati.

25Kwenye mulango wa kuingilia kwenye baraza kulichorwa makerubi na miti ya ngazi kama ilivyokuwa kwenye kuta. Na kulikuwa kifuniko cha ubao kikifunika mulango kwa inje kwenye sehemu ya kuingilia ndani.

26Pembeni ya chumba hiki, kulikuwa madirisha madogo na kuta zilipambwa kwa michoro ya miti ya ngazi.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help