Zaburi 64 - Swahili Congo Revised Bible 2002

Kuomba ulinzi wa Mungu

1Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo.

2Ee Mungu,

usikilize malalamiko yangu.

Uyalinde maisha yangu kutoka vitisho vya waadui.

3Unikinge na shauri baya la waovu,

nayo fujo ya watu wabaya.

4Wananoa ndimi zao kama upanga,

nayo maneno yao ni makali kama mishale.

5Wanapiga mutu mukamilifu kwa uficho,

wanamupiga kwa rafla bila kuogopa.

6Wanashirikiana katika nia yao mbaya;

wanapatana pahali pa kuficha mitego yao.

Wanajisemesha: “Hakuna atakayeweza kuiona.”

7Wanafanya shauri baya wakijisemesha:

“Tumetimiza sasa mipango yetu!

Nani anayeweza kugundua mafikiri ya ndani ya mutu?”

8Lakini Mungu atawapiga mishale,

na kuwaumiza kwa rafla.

9Atawaangamiza kwa sababu ya maneno yao;

kila atakayewaona atatikisa kichwa.

10Hapo watu wote wataogopa;

watatangaza kazi Mungu aliyoifanya,

na kufikiri juu ya matendo yake.

11Watu wa haki watamufurahia Yawe,

na kukimbilia kwake;

watu wote wenye moyo wa usawa watamusifu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help