Wimbo wa Solomono 4 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Hakika sura yako ni nzuri, ewe mupenzi wangu,

hakika sura yako ni nzuri!

Macho yako ni mazuri kama ya njiwa

ndani ya ushungi wako.

Nywele zako ni kama kundi la mbuzi

wanaoshuka kwenye milima ya Gileadi.

2Meno yako ni kama kundi la kondoo dike waliokatwa manyoya,

wanaotoka kwenye maji kisha kuogeshwa;

kila mumoja akiwa na pacha lake,

na hakuna yeyote aliyekufiwa.

3Midomo yako ni kama utepe mwekundu,

kinywa chako kinapendeza kweli.

Mashavu yako ni kama nusu mbili za makomamanga

ndani ya ushungi wako.

4Shingo yako ni kama munara wa Daudi,

uliojengwa kwa kulinda silaha,

ambako ngao elfu moja zimetundikwa,

zote zikiwa za mashujaa.

5Maziba yako ni kama paa mapacha,

ambao wanachungwa penye yungiyungi.

6Nitakaa kwenye mulima wa marasi,

na kwenye kilima cha ubani,

mpaka pale kutakapopambazuka,

na giza kutoweka.

7Wewe ni nzuri kabisa, ee mupenzi wangu,

wewe hauna kilema chochote.

8Kuja, muchumba wangu, tuondoke Lebanoni,

na tuiache mbali milima ya Lebanoni.

Shuka toka kilele cha mulima Amana,

toka kilele cha Seniri na Hermoni,

toka mashimo ya simba,

toka kwenye milima ya chui.

9Umeua moyo yangu, dada yangu, muchumba wangu,

umeua moyo yangu,

kwa kunitupia jicho mara moja tu,

na kwa ule mukufu wako katika shingo.

10Dada yangu, muchumba wangu;

mapendo yako yananivuta ajabu.

Ni bora kuliko divai,

marasi yako yananuka vizuri kuliko viungo vyote.

11Midomo yako inadondosha asali, ee muchumba wangu,

ulimi wako una asali na maziwa.

Harufu nzuri ya nguo zako ni kama miti ya Lebanoni.

12Dada yangu, muchumba wangu,

ni bustani yangu ya pekee,

chemichemi inayochungwa.

13Machipukizi yako ni bustani ya mikomamanga

pamoja na matunda bora kuliko yote,

hina na nardo,

14nardo na zafarani, muchai na mudalasini,

ubani na udi,

na mimea mingine yenye harufu nzuri.

15Wewe ni chemichemi ya bustani,

kisima cha maji yasiyokauka,

vijito vinavyotiririka kutoka milima ya Lebanoni.

Masemi ya muke

16Vuma, ewe upepo wa kaskazini,

kuja, ewe upepo wa kusini,

muvume juu ya bustani yangu,

mujaze anga kwa marasi,

mupenzi wangu akuje katika bustani yake

akule matunda yake bora kuliko yote.

Masemi ya mume
Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help