1Kristo aliteswa kimwili. Basi ninyi vilevile mujikaze mupate kuwa na nia kama ile yake. Kwa maana mutu anayevumilia mateso ya mwili, anaachana kabisa na zambi.
2Sasa, musiishi tena kufuatana na tamaa za kimutu, lakini muishi kufuatana na mapenzi ya Mungu kwa muda unaowabakilia kwa kukaa katika dunia.
3Kufuatana na hiyo, zamani mulipitisha siku nyingi mukifanya matendo yanayolingana na ya wapagani. Mulizoea kuishi katika uasherati, tamaa mbaya, ulevi, karamu za ulafi, za ulevi na kuabudu sanamu.
4Sasa, wapagani wanashangaa kuona ninyi hamushirikiani nao tena katika maisha ya ovyo ovyo; na kwa hiyo wanawasingizia ninyi.
5Lakini watu hawa watasamba maneno yao mbele ya Mungu anayekwisha kuwa tayari kwa kuhukumu wafu na wazima.
6Kwa sababu hiyo Habari Njema ilitangazwa kwa wafu, kwa wale waliohukumiwa kimwili sawa watu wengine, kusudi wapate kuishi kiroho kama vile Mungu anavyoishi.
Namna waamini wanapaswa kutumia zawadi za kiroho7Mwisho wa vitu vyote unakaribia kutimia. Kwa hiyo mukuwe wenye akili na waangalifu, kusudi mukuwe na uwezo wa kuomba.
8Na zaidi ya yote mudumu katika upendo ninyi kwa ninyi, maana upendo unafunika zambi nyingi.
9Mukaribishane ninyi kwa ninyi pasipo kunungunika.
10Kila mutu kati yenu anapaswa kuitumia zawadi ya kiroho aliyojaliwa na Mungu kwa ajili ya mafaa ya wengine. Na hivi mutakuwa walinzi wazuri wa zawadi mbalimbali mulizopewa na Mungu.
11Yule anayehubiri, anapaswa kutoa ujumbe wa Mungu. Na yule anayetumika, atumike kwa kadiri ya nguvu alizopewa na Mungu, kusudi Mungu atukuzwe katika mambo yote kwa njia ya Yesu Kristo anayekuwa mwenye utukufu na uwezo kwa milele na milele. Amina.
Mateso ya mukristo12Wandugu wapendwa, musishangae kwa kuona mateso makubwa ya kuwajaribu munayopata. Musiyahesabu kuwa kitu kigeni kwenu.
13Lakini mufurahi kwa sababu munashiriki katika mateso ya Kristo. Na kwa hiyo mutashangilia kwa furaha wakati atakapoonekana katika utukufu.
14Ninyi ni wenye heri kama watu wakiwatukana kwa ajili ya Kristo, kwa kuwa Roho wa utukufu, maana yake Roho wa Mungu anakaa ndani yenu.
15Kati yenu kusikuwe hata mutu mumoja anayeteswa kwa sababu yeye ni mwuaji, mwizi, mutenda mabaya au mwenye kujiingiza katika mambo ya watu wengine.
16Lakini mutu akiteswa kwa sababu yeye ni mukristo, asione haya, lakini atukuze Mungu kwa kuwa anaitwa kwa jina lile.
17Wakati wa hukumu unakaribia. Na hukumu itaanza na watu wa Mungu. Na kama hukumu inaanzia kwetu sisi, basi mwisho wake utakuwa namna gani kwa wale wasiotii Habari Njema ya Mungu?
18Ni kama vile Maandiko haya Matakatifu yanavyosema:
“Ikiwa hata kuokolewa kwa mwenye haki ni kugumu;
itakuwa namna gani kwa mwovu na mwenye zambi?”
19Basi watu wanaoteswa kwa ajili ya kufanya mapenzi ya Mungu, waendelee kutenda mema, nao watoe roho yao katika mikono ya Mungu Muumba wao anayekuwa mwaminifu kabisa.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.