1Wimbo wa Solomono unaokuwa bora kuliko nyimbo zote. Shairi la kwanzaMasemi ya muke
2Heri midomo yako ingalinibusu,
maana mapendo yako ni bora kuliko divai.
3Manukato yako yananuka vizuri,
na jina lako ni kama marasi yenye harufu nzuri.
Kwa hiyo wabinti wote wanakupenda!
4Unipeleke, tuende haraka,
mufalme amenileta katika chumba chake.
Tutafurahi na kukushangilia pamoja,
tutasifu mapenzi yako kuliko divai.
Wabinti wana haki ya kukupenda!
5Enyi wabinti wa Yerusalema,
mimi ni mweusi.
Ninapendeza kama mahema ya Kedari,
kama mapazia ya nyumba ya Solomono.
6Musinishangae kwa sababu mimi ni mweusi.
Ni kwa sababu jua limenichoma.
Wandugu zangu walinikasirikia,
wakanifanya kuwa mutumishi katika mashamba ya mizabibu.
Lakini sikuchunga shamba langu la mizabibu.
7Basi uniambie ee wangu wa moyo,
utawakulishia kondoo wako wapi?
Ni wapi watakapopumzikia pa saa sita?
Kwa nini mimi nikutafute
kati ya makundi ya wenzako?
Masemi ya mume8Ewe unayependeza kuliko wanawake wote;
kama haujui, fanya hivi:
ufuate nafasi kondoo walipopita;
basi, uwakulishie mbuzi wako karibu na hema za wachungaji.
9Wewe ee mupenzi wangu,
ninakulinganisha na farasi dume wa magari ya Mufalme wa Misri.
10Pete za masikio
zinapendeza mashavu yako.
Mikufu ya mawe ya bei kali
inapendeza shingo yako.
11Tutakufanyizia mikufu ya zahabu,
iliyopambwa vizuri kwa feza.
Masemi ya muke12Mufalme alipokuwa akiikaa kwenye meza yake,
marasi yangu ya nardo yalisambaa kila pahali.
13Mupenzi wangu ni kama mufuko wa ubani kwangu,
kati ya maziba yangu.
14Mupenzi wangu ni kama maua ya hina yanayochanua
kwenye mashamba ya mizabibu kule Engedi.
Masemi ya mume15Hakika sura yako ni nzuri, ee mupenzi wangu,
hakika sura yako ni nzuri!
Macho yako ni kama ya njiwa!
Masemi ya muke16Hakika sura yako ni nzuri, ewe ninayekupenda,
sura yako ni nzuri kweli!
Majani mabichi yatakuwa kitanda chetu;
17miti ya mierezi itakuwa nguzo za nyumba yetu,
na miti ya miberoshi itakuwa dari yake.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.