1Yawe akamwambia Musa:
2Uwaambie Waisraeli wote pamoja hivi: Mukuwe watakatifu maana mimi Yawe, Mungu wenu, ni mutakatifu.
15Unapotoa hukumu uamue kwa haki, usimupendelee masikini wala kumwogopa mwenye cheo. Lakini hukumu mwenzako kwa haki.
19Unapaswa kuyashika masharti yangu. Usiiache mifugo yako ipandiwe na nyama wa aina nyingine. Usipande mbegu za aina mbili katika shamba lako. Usivae nguo iliyofumwa kwa aina mbili za nguo.
20Mwanaume akilala na mwanamuke mujakazi ambaye amechumbiwa na mwanaume mwingine, lakini bado hajakombolewa wala kupewa uhuru, uchunguzi ufanywe. Lakini wasiuawe kwa sababu mwanamuke huyo hakukuwa bado huru.
21Mwanaume huyo ataleta mbele ya hema la mukutano sadaka yake ya kondoo dume kwa ajili ya kosa na kunitolea mimi Yawe.
22Kuhani atamufanyia ibada ya upatanisho kwa kutumia kondoo huyo mbele ya Yawe kwa ajili ya zambi aliyotenda, naye atasamehewa zambi hiyo aliyotenda.
23Mutakapofika katika inchi ya Kanana na kupanda aina zote za miti ya matunda, matunda hayo hamutayakula. Hamutaruhusiwa kuyakula kwa muda wa miaka mitatu.
24Katika mwaka wa ine matunda yake yote yatakuwa matakatifu, yatatolewa kuwa sadaka ya sifa, kwa Yawe.
25Lakini matunda ya kuanzia mwaka wa tano hayo munaweza kuyakula na mavuno yenu yataongezeka. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.
26Musikule nyama yoyote pamoja na damu. Musifanye ulozi wala kuaguza.
31Musiwaendee waaguzi wa mizimu wala wachawi kwa kuwaomba wawaaguzie. Mukifanya hivi, mutajichafua. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.
32Unapokuwa mbele ya muzee unapaswa kusimama kwa kumupa heshima yake, nawe umwogope Mungu wako. Mimi ni Yawe.
33Kama kuna mugeni katika inchi yako usimutendee vibaya. Ang. Kut 22.21; Kumb 24.14-18; 27.19
34Huyo mugeni anayekaa nawe atakuwa kwako kama vile mwenyeji nawe utamupenda kama vile unavyojipenda mwenyewe, kwa sababu nawe ulikuwa mugeni katika inchi ya Misri. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.
35Usikose kuamua kwa haki juu ya vipimo vya urefu, uzito na ujazo. Ang. Kumb 25.13-16; Mez 20.10; Eze 45.10
36Munapaswa kutumia mizani ya kweli na vipimo vinavyokuwa vya kweli. Mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyewatoa katika inchi ya Misri.
37Munapaswa kushika na kutimiza masharti yangu na maagizo yangu. Mimi ni Yawe.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.