Hesabu UTANGULIZI - Swahili Congo Revised Bible 2002
UTANGULIZIJina la kitabu hiki: Hesabu, linatokana na hesabu mbili za watu ambazo zinatajwa katika kitabu chenyewe. Katika kitabu hiki tunaelezwa jinsi Musa alivyowahesabu Waisraeli mbele ya kuanza safari yao kutoka mulima Sinai, na tena nyuma katika inchi ya Moabu, upande wa mashariki wa Yordani. Kitabu chenyewe kinaeleza jinsi Waisraeli, nyuma ya kupokea maagizo yote ya Mungu kule Sinai, wakasafiri katika jangwa kuelekea inchi ya ahadi (1.1–10.10). Kwanza walifika Kadesi Barnea upande wa kusini wa inchi hiyo, lakini hawakuweza kuingia. Hivyo ikawapasa kukaa katika jangwa miaka makumi ine muda ambapo walijitayarisha na kwa mwisho wakaikamata inchi ya Moabu upande wa mashariki wa bahari ya Chumvi (10.11–21.35). Sura za mwisho za kitabu hiki zinasimulia juu ya matukio yaliyoelekea kutekwa kwa inchi ya Moabu; kutoka humo Waisraeli wakaingia katika inchi waliyoahidiwa (22.1–36.13).Kitabu hiki ambacho kinafuata vile vya Mwanzo, Kutoka na Walawi kinatupatia picha ya Waisraeli katika hali yao kweli ya kibinadamu – wenye matumaini na mashaka, wenye nguvu na uzaifu. Kinaonyesha vilevile uaminifu wa Mungu katika kuwalinda watu wake.