1Enyi Waisraeli, musikilize neno Yawe alilosema juu yenu, enyi taifa zima alilolitoa katika inchi ya Misri:
2Kati ya mataifa yote katika ulimwengu,
ni ninyi tu niliowachagua.
Kwa hiyo nitawaazibu ninyi,
kwa sababu ya uovu wenu wote.
Madaraka ya nabii3Watu wawili wanaweza kusafiri pamoja
bila kupatana kwanza?
4Simba ananguruma katika pori
kama hajapata nyama?
Simba mukali ananguruma katika pango lake
kama hajakamata kitu?
5Mutego bila chambo
utamunasa ndege?
Mutego unaweza kufyatuka
bila kuguswa na kitu?
6Baragumu ya vita inalia katika muji
bila kutia watu hofu?
Muji unaweza kupatwa na hasara
ambayo haikuletwa na Mungu?
7Hakika, Bwana wetu Yawe hafanyi kitu
bila kuwafunulia watumishi wake manabii nia yake.
8Simba akinguruma,
ni nani asiyeogopa?
Bwana wetu Yawe akisema,
ni nani atakataa kuutangaza ujumbe wake?
Kuangamizwa kwa Samaria9Mutangaze katika nyumba nzuri kule Asidodi,
na katika nyumba nzuri za inchi ya Misri:
Mukusanyike kwenye milima
inayoizunguka inchi ya Samaria,
mujionee fujo kubwa
na mateso yanayofanyika kule.
10Hawajui kabisa kutenda mambo yanayokuwa sawa!
–Ni ujumbe wa Yawe.–
Wamejaza nyumba zao nzuri na
vitu vya wizi na mateso.
11Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi:
Waadui wataizunguka inchi yenu,
wataharibu kuta zako,
na kuziteka nyumba zao nzuri.
12Yawe, anasema hivi: Kama vile muchungaji anavyonyanganya toka katika kinywa cha simba miguu miwili tu au kipande cha sikio la kondoo, ndivyo watu wachache tu wa Israeli wanaoishi Samaria, ambao sasa wanalalia vitanda vizuri na matandiko ya hariri watakavyobaki.
13Musikilize, muwaonye wazao wa Yakobo.
–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe, Mungu wa majeshi.–
14Siku nitakapowaazibu Waisraeli
kwa sababu ya makosa yao,
nitayaharibu vilevile mazabahu ya muji wa Beteli.
Nitazikata pembe za kila mazabahu
na kuziangusha chini.
15Nitaziharibu nyumba zote katika muji na katika vijiji;
nitazibomoa nyumba zilizopambwa kwa pembe za tembo,
nyumba kubwakubwa zitaanguka.
–Ni ujumbe wa Yawe.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.