Yobu 40 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Yawe akaendelea kumwambia Yobu:

2Wewe mwenye kuchunguza makosa utashindana na Mungu Mwenye Uwezo?

Wewe unayebishana nami Mungu, basi ujibu mambo hayo!

3Kisha Yobu akamujibu Yawe:

4Mimi sifai kitu. Nitakujibu nini?

Ninafunga kinywa changu.

5Nilisubutu kusema na sitasema tena.

Nilisema mengi lakini sitaendelea kusema zaidi.

6Halafu Yawe akamujibu kutoka katika zoruba:

7Ujikaze kama mwanaume.

Nitakuuliza, nawe utanijibu.

8Unataka kweli kugeuza hukumu yangu,

kuniona nina kosa kusudi wewe usikuwe na kosa?

9Una nguvu kama mimi Mungu?

Unaweza kunguruma kwa sauti kama yangu?

10Basi, ujionyeshe kuwa na utukufu na ukubwa,

ujipambe kwa heshima na mamlaka.

11Uwamwangie watu hasira yako kubwa;

umwangalie kila mwenye kiburi na kumwangusha.

12Umwangalie kila mwenye kiburi na kumuporomosha,

uwakanyage waovu pahali wanapokuwa.

13Uwazike wote pamoja ndani ya udongo;

umufunge kila mumoja kwa kifungo cha kifo.

14Halafu nitakutambua

kwa vile nguvu yako mwenyewe imekupa ushindi.

15Uangalie yule nyama mukubwa kiboko.

Nilimwumba kama nilivyokuumba wewe.

Yeye anakula majani kama ngombe,

16lakini ana nguvu ajabu katika mwili wake,

na mishipa ya tumbo lake ni imara.

17Mukia wake ni wenye nguvu kama mwerezi,

mishipa ya mapaja yake imeshonwa pamoja.

18Mifupa yake ni kama mirija ya shaba,

mbavu zake ni kama vipande vya chuma.

19Yeye ni wa kwanza wa ajabu kati ya viumbe vyangu!

Ni mimi Muumba wake ninayeweza kumutawala.

20Milima ambamo nyama wote wa pori wanamochezea

inatoa chakula chake.

21Anajilaza chini ya vichaka vya miiba,

na kujificha kati ya matete ndani ya tingitingi.

22Vivuli vya vichaka vya miiba vinamufunika

na vya miti inayoota pembeni ya vijito.

23Muto ukifurika haogopi,

hatishiki hata muto Yordani ukifurikia katika kinywa.

24Nani anayeweza kuziba macho yake na kumuteka?

Nani anayeweza kumutoboa pua kwa mutego?

25Unaweza kuvua yule nyama mukubwa Leviatani kwa ndoana,

au kuufunga ulimi wake kwa kamba?

26Unaweza kumutia kamba katika pua lake,

au kumutoboa taya kwa kulabu?

27Unazani atakusihi umwachilie?

Atazungumuza nawe kwa upole?

28Atafanya mapatano nawe,

umuchukue kuwa mutumishi wako milele?

29Utacheza naye kama ndege,

au kumufunga kamba acheze na wajakazi wako?

30Unazani wavuvi watashindania bei yake?

Wachuuzi watasubutu kumukata na kugawanyana?

31Wanaweza kuitoboa ngozi yake kwa mikuki,

au kichwa chake kwa chuma cha kuvua samaki?

32Jaribu tu kumugusa: ukifikiri juu ya vita naye,

hautarudilia tena kufanya hivyo.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help