1Waisraeli walikuwa wameapa kule Misipa kwamba hakuna hata mumoja kati yao ambaye angemwachilia binti yake aolewe kwa watu wa kabila la Benjamina.
2Basi, wakaenda mpaka Beteli wakakaa kule mbele ya Mungu mpaka magaribi. Wakalalamika kwa sauti na kulia kwa uchungu mwingi.
3Wakasema: “Ee Yawe, Mungu wa Israeli, kwa nini jambo hili limetukia hata tupungukiwe na kabila katika Israeli?”
4Kesho yake watu wakaamuka mapema, wakajenga mazabahu, wakatoa sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka za amani.
5Kisha wakaulizana: “Kati ya makabila yote ya Israeli kuna kikundi chochote ambacho hakikuhuzuria mukutano uliofanyika mbele ya Yawe?” Walikuwa wamefanya kiapo kwamba mutu yeyote ambaye hatahuzuria mbele ya Yawe kule Misipa anapaswa kuuawa.
6Lakini Waisraeli wakawaonea huruma wandugu zao wa kabila la Benjamina, wakasema: “Leo kabila moja la Israeli limeangamia.
7Sasa tutafanya nini kwa kuwapatia wanawake hao wanaume wa kabila la Benjamina waliobaki kwa vile tulikwisha kuapa kwa jina la Yawe kwamba hatutawapa wabinti zetu wakuwe wake zao?”
8Wakataka kujua kama kulikuwa kikundi chochote cha makabila ya Israeli ambacho hakikuhuzuria mukutano mbele ya Yawe kule Mispa. Wakagundua kwamba hakuna mutu yeyote kutoka Yabesi-Gileadi aliyekuja kwenye mukutano ule.
9Waisraeli walipohesabiwa kule Misipa hakuna mukaaji yeyote wa Yabesi-Gileadi aliyehuzuria.
10Kwa hiyo Waisraeli wakapeleka watu wake elfu kumi na mbili elfu wanaokuwa hodari kabisa na kuwaamuru: “Muende muwaue wakaaji wa Yabesi-Gileadi; wanawake pamoja na watoto.
11Mutawaua wanaume wote na wanawake wote wasiokuwa mabikira.”
12Basi wakakuta kati ya wakaaji wa Yabesi-Gileadi wabinti mia ine ambao hawakukuwa wamekwisha kulala na mwanaume yeyote, wakawapeleka katika kambi kule Shilo katika inchi ya Kanana.
13Kisha wote pamoja wakawapelekea ujumbe wa amani watu wa kabila la Benjamina ambao walikuwa kwenye mulima wa Rimoni.
14Wanaume hao wa kabila la Benjamina wakawarudilia hao wenzao wakati uleule. Basi wakapewa wale wanawake ambao walikuwa wameachwa kule Yabesi-Gileadi. Lakini wanawake hao hawakuwatosha.
15Waisraeli wakawaonea huruma watu wa kabila la Benjamina, maana Yawe alisababisha kukuwe shimo kati ya Waisraeli.
16Kisha wazee wa Israeli wakasema: “Sasa tutafanya nini kwa kuwapatia wake hao wanaume waliobaki kwa vile wanawake wote wa kabila la Benjamina waliangamia?
17Inafaa wanaume waliobaki wa kabila la Benjamina wapewe wanawake kusudi waendeleshe kabila, na hivyo kusipotee kabila lolote katika Israeli.
18Lakini hatuwezi kuwatoa wabinti zetu wakuwe wake zao, maana tulikwisha kuapa kwamba mutu yeyote atakayemwoesha binti yake kwa mwanaume wa kabila la Benjamina alaaniwe.”
19Basi wakakumbuka kwamba sikukuu ya Yawe iliyofanyika kila mwaka kule Shilo, muji unaokuwa upande wa kaskazini wa Beteli, kwenye njia kubwa inayotoka Beteli kwenda Sekemu, ilikuwa inakaribia.
20Kwa hiyo wakawaamuru wale wanaume wa kabila la Benjamina: “Muende muvizie na kufichama katika mashamba ya mizabibu.”
21Mukuwe macho. Wabinti wa Shilo watakapotoka inje kwa kucheza wakati wa sikukuu, mutoke kwenye mizabibu na kila mutu ajikamatie binti mumoja akuwe muke wake. Kisha murudi katika inchi ya Benjamina.
22Baba zao au kaka zao wakikuja kutulalamikia tutawaambia: “Sisi tunawaomba muwahurumie watu wa Benjamina na kuwaacha watwae hao wanawake; maana hatukupata wanawake wa kutosha katika vita ya Yabesi-Gileadi. Na kwa sababu si ninyi wenyewe muliowapatia hao wabinti zenu, hamutahukumiwa kwamba mumevunja kiapo.”
23Wale wanaume wa kabila la Benjamina wakafanya hivyo, kila mumoja akajichagulia binti kati ya wabinti waliotoka inje kwa kucheza kule Shilo na kumutwaa kuwa muke wake. Kisha wakarudi katika eneo lao, wakaijenga miji yao upya na kuishi mule.
24Wakati uleule Waisraeli wakaondoka, kila mutu akarudi katika eneo la kabila lake na jamaa yake. Kila mutu akarudi katika sehemu aliyogawanyiwa.
25Siku hizo hakukukuwa mufalme katika Israeli. Kila mutu alifanya sawa vile alivyotaka.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.