1Neno la Yawe lilimufikia Yona mara ya pili kusema hivi:
2Simama, uende Ninawe, ule muji mukubwa, uwatangazie watu ujumbe ninaokupa.
3Basi, Yona akaondoka, akaenda Ninawe kama vile Yawe alivyomwagiza.
Muji wa Ninawe ulikuwa mukubwa sana. Upana wake ulikuwa mwendo wa siku tatu.
4Alipofika, Yona aliingia katika muji. Kisha kutembea mwendo wa siku nzima, akaanza kutangaza: Kunabaki siku makumi ine tu na muji huu wa Ninawe utaangamizwa!
5Basi, watu wa Ninawe wakauamini ujumbe wa Mungu, wakatangaza kufunga kula chakula, na kwamba kila mumoja wao, mukubwa kama vile mudogo, avae gunia.
6Habari hizi zikamufikia mufalme wa Ninawe, naye akaondoka juu ya kiti chake cha kifalme, akavua nguo yake ya kifalme, akavaa gunia na kuikaa katika majivu.
7Kisha mufalme akawatangazia wakaaji wa Ninawe: Mimi mufalme, pamoja na wakubwa wangu, ninatoa amri hii: Kusikuwe mutu yeyote, ngombe au nyama yeyote wa kufugwa, atakayeonja kitu chochote. Hairuhusiwi kwa mutu yeyote au nyama kula au kunywa.
8Watu wote na nyama wavae gunia. Kila mutu amwombe Mungu na kumusihi kwa moyo. Kila mumoja aache uovu wake, aache kutenda kwa ukali.
9Labda Mungu atabadilisha nia yake, na kuacha kutukasirikia, nasi hatutaangamizwa!
10Mungu alipoona walivyofanya, na jinsi walivyouacha uovu wao, akabadilisha nia yake, akaacha kuwatenda kama alivyokuwa amekusudia.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.