1Ninataka mujue jinsi ninavyofanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu, kwa ajili ya waamini wa Laodikia na kwa ajili ya wote ambao hawajapata kuniona bado.
2Ninapigana kusudi wapate kuwa na bidii na kuungana katika upendo. Na zaidi ya hii wapate kuwa na uhakika kabisa unaotokana na ufahamu mukamilifu. Hivi wataweza kujua siri ya Mungu, maana yake kumujua Kristo mwenyewe,
3kwa maana hazina zote za hekima na elimu zimefichwa ndani yake.
4Ninawaambia ninyi maneno haya kusudi mutu asiwadanganye kwa maneno matamu ya kupotosha.
5Ijapokuwa mimi ni mbali nanyi kwa mwili, lakini mimi ni pamoja nanyi kwa roho, nami ninafurahi kuona namna munavyoishi katika utaratibu muzuri na kusimama imara katika imani mbele ya Kristo.
Kujenga maisha juu ya Kristo6Basi kwa sababu mumemukubali Kristo kuwa Bwana wenu, muishi katika kuungana naye.
7Mukuwe na mizizi ndani yake, mujijenge juu yake na kusimama imara katika imani sawa vile mulivyofundishwa. Na zaidi ya hii mukuwe wenye kushukuru sana.
8Mujiangalie hata mutu asiwapotoshe kwa elimu yake ya udanganyifu mutupu inayotegemea desturi za watu na roho mbaya zinazotawala dunia, lakini haitegemei mafundisho ya Kristo.
9Kwa maana ukamilifu wote wa Mungu uko ndani ya Kristo katika mwili wake.
10Na kwa kuungana naye, ninyi mumepata kukamilika. Yeye ndiye anayetawala roho zote zenye mamlaka na uwezo.
11Katika kuungana naye, mumetahiriwa wala si kwa mikono ya watu, lakini mumetahiriwa na Kristo, na kutahiriwa kule kumewakomboa toka katika hali zaifu ya kimwili.
12Kwa maana mumezikwa pamoja na Kristo kwa njia ya ubatizo, nanyi mumefufuliwa vilevile pamoja naye, kwa sababu mumeamini uwezo wa Mungu, aliyemufufua.
13Zamani mulikuwa mumekufa kwa sababu ya zambi zenu na kwa sababu mulikuwa watu wa mataifa mengine, wasiotahiriwa. Lakini sasa, Mungu amewapatia ninyi uzima pamoja na Kristo, naye ametusamehe zambi zetu zote.
14Alifuta barua ya madeni yetu na sherti zilizotushitaki. Aliyafuta kabisa kwa kuyapigilia juu ya musalaba.
15Mungu alinyanganya uwezo wa wakubwa na wenye mamlaka, naye akawaonyesha waziwazi, akiwatembeza kama wafungwa katika maandamano ya ushindi wa Mwana wake.
16Basi, mutu asiwahukumu juu ya chakula au kinywaji, au juu ya kushika sikukuu fulani, ikiwa sikukuu ya Mwandamo wa Mwezi au siku ya Sabato.
17Mambo hayo yote ni kivuli cha mambo yatakayokuja, lakini ukweli wa mambo yote ni Kristo mwenyewe.
18Musikubali kuhukumiwa na mutu yeyote anayejionyesha kwa inje kuwa yeye ni munyenyekevu na mwenye kuabudu malaika. Mutu wa namna hii anatia sana maana juu ya maono anayopata, naye anajitapa bure juu ya mafikiri yake ya kimutu.
19Mutu yule hashikamani na Kristo anayekuwa kichwa cha mwili. Chini ya uongozi wa Kristo, mwili muzima unakulishwa vizuri na kuunganishwa pamoja kwa njia ya maunganio na vifundo vyake, kusudi upate kukomaa kufuatana na mapenzi ya Mungu.
Tusifuate kanuni zilizotungwa na watu20Ninyi mumekufa pamoja na Kristo na kukombolewa toka katika uwezo wa roho mbaya zinazotawala dunia. Kwa nini munaishi tena kama watu wa dunia mukilazimishwa kushika kanuni kama hizi:
21“Usikule hiki”, “Usionje hiki,” “Usiguse hiki na hiki!”
22Mambo hayo yote yanaelekea vitu vyenye kuharibika mara moja tu vinapotumiwa. Navyo vyote ni kanuni na mafundisho ya watu tu.
23Hakika kanuni hizi zinaonekana kama za hekima kwa maana zinatokana na ibada ya kipekee ya watu wale pamoja na unyenyekevu wao na shurti zao za kuutesa mwili. Lakini hazifai kitu kwa kuzuiza tamaa za mwili.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.