Yobu 20 - Swahili Congo Revised Bible 2002

1Kisha Zofari wa inchi ya Namati akajibu:

2Mafikiri yangu yananisukuma nikujibu,

wala siwezi kujizuia tena.

3Ninasikia maonyo nisiyoweza kuvumilia,

lakini akili yangu inanisukuma nijibu.

4Wewe labda umesahau jambo hili:

kwamba tangu zamani Mungu alipomwumba mutu katika dunia,

5mwovu atajiona ameshinda kwa muda tu,

furaha ya asiyemwogopa Mungu ni ya muda mufupi tu!

6Mwovu akiweza kupanda hata kufikia mbingu,

na kichwa chake kufika kwenye mawingu,

7atatupiliwa mbali kama mavi yake.

Waliopata kumujua watajiuliza: “Yuko wapi?”

8Atatoweka kama ndoto, asionekane tena,

atafutikana kama maono ya usiku.

9Aliyemwona, hatamwona tena,

wala pale alipoishi hapatatambuliwa tena.

10Yeye mwenyewe atarudisha mali yake yote,

watoto wake wataomba huruma kwa wamasikini.

11Japo alijisikia amejaa nguvu ya ujana,

lakini italala pamoja naye katika mavumbi.

12Katika kinywa chake uovu ni mutamu kama sukari,

anauficha chini ya ulimi wake;

13hataki kabisa kuuachilia,

lakini anaushikilia katika kinywa chake.

14Lakini unapofika ndani ya tumbo unakuwa muchungu,

mukali kama sumu ya nyoka.

15Mwovu anameza mali haramu na kuitapika;

Mungu anaitoa ndani ya tumbo lake.

16Ananyonya sumu ya nyoka

na nyoka atamuuma na kumwua.

17Hataona tena mitiririko

ya asali na ya maziwa.

18Ataacha matunda ya jasho lake.

Hatakuwa na uwezo wa kuyaonja,

19kwa sababu amewaangamiza wamasikini na kuwaachilia,

amenyanganya nyumba ambazo hakuzijenga.

20Kwa vile ulafi wake hauna mwisho,

hataweza kuokoa kitu chochote cha lazima.

21Kisha kula hakuacha hata makombo.

Kwa hiyo fanaka yake yote haitadumu.

22Atakapotajirika sana atapatwa na taabu,

hasara itamupata kwa nguvu zote.

23Akiwa anajishugulisha kwa kushibisha tumbo,

Mungu atamuletea kasirani yake

imutiririkie kama chakula chake.

24Labda ataweza kuepuka upanga wa chuma,

kumbe atachomwa na upanga wa shaba.

25Mushale utachomolewa kutoka katika mwili wake;

incha yake itatolewa katika mugongo wake ikingaa,

vitisho vya kifo vitamupata.

26Hazina zake zitaharibiwa,

moto wa ajabu utamuteketeza;

kilichobaki katika nyumba yake kitateketezwa.

27Mbingu zitafichua uovu wake,

dunia itajitokeza kumushambulia.

28Mali zake zitanyanganywa

katika siku ya kasirani ya Mungu.

29Hii ndiyo sehemu ya mutu mwovu kutoka kwa Mungu,

ndio mwisho aliopangiwa na Mungu.

Jibu la Yobu
Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help