Hosea UTANGULIZI - Swahili Congo Revised Bible 2002

UTANGULIZIHosea aliitwa kuwa musemaji wa Mungu katika ufalme wa kaskazini wa Israeli, katika mwaka wa 750-725 mbele ya Kristo. Alitanguliwa na nabii Amosi ambaye vilevile alihubiri katika ufalme wa kaskazini wa Israeli.Hosea analaumu vikali ibada za miungu ya uongo na ukosefu wa imani kwa Mungu kati ya Waisraeli. Hali hiyo ya kumwasi Mungu, Hosea anaieleza kwa picha ya maisha yake ya ndoa. Kama vile muke wake Gomeri alivyomugeuka na kuacha kuwa mwaminifu, ndivyo watu walivyomwacha Mungu. Kwa sababu hiyo, watu wa Israeli wataazibiwa. Hata hivyo, kwa mwisho, Mungu, kwa upendo wake mukubwa, atawarudisha na kuleta tena uhusiano wake nao.Sura 1-3 inaeleza juu ya maisha ya ndoa ya Hosea na muke wake ambayo ni mufano wa uasi wa Waisraeli kwa Mungu. Hosea anatangaza hukumu ya Mungu kwa watu wote, lakini anaonyesha vilevile kwamba kwa mwisho upendo wa Mungu utashinda.Sura 4-14 inaelekea mahubiri mengine ya nabii.
Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help